Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, ningependa kuchangia kama ifuatavyo. Nashauri Serikali kuhakikisha haki na amani inalindwa na itambue amani ni tunda la haki. Pale tu ambapo Polisi watatenda haki ndipo amani itashamiri Tanzania. Mfano, Polisi wanapozuia vikao vya ndani kwa Upinzani wakati Chama Tawala wakifanya vikao, hiyo siyo haki. Nimeshuhudia kwa macho yangu nikiwa kwenye kikao cha ndani Kibaha, nikiambiwa kuvunja kikao hicho eti kutatokea vurugu wakati ni kikao cha Kikatiba cha chama.

Mheshimiwa Spika, nishauri Serikali ifuatilie rushwa zinazoendelea kwa Askari wa Usalama Barabarani. Mfano, magari yanayotoka Saba Saba kuelekea Nane Nane, siku moja kwa macho yangu nimeona Polisi wanasimama Kilimo Kwanza kila daladala wanatoa Sh.2,000, hivyo halikaguliwi linaendelea na safari hata kama kuna shida kwenye gari.

Mheshimiwa Spika, Serikali iangalie kwa upya maisha ya Askari Magereza na Polisi, makazi yao siyo rafiki. Hawawezi kufanya kazi zao kwa weledi kama Serikali haitawaangalia kwa jicho la ziada.

Mheshimiwa Spika, niombe Serikali iangalie ajira za Polisi kwani zinatolewa kwa upendeleo bila kujali sifa tarajiwa za Polisi zilizoainishwa katika ajira hizo.