Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kuwa na hali ya uzima na afya. Pia namshukuru kuwa na uhai na uzima wa kusimama kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Mambo ya Ndani.

Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake kwa jitihada kubwa wanazozichukua kufanya kazi zao hizi za Wizara ya Mambo ya Ndani. Naendelea kuzungumzia suala la amani na utulivu na usalama. Wenzangu wengi waliosimama wamezungumzia suala hili lakini kila mmoja kazungumzia kwa mtazamo wake.

Mheshimiwa Spika, mtazamo wangu ninaouzungumzia ni kwamba usalama, amani, utulivu umeimarika, Jeshi la Polisi wanafanya kazi kubwa sana kuhusu suala hili la amani na utulivu. Hivi sasa hatuna wasiwasi wa kwamba nina safari yangu hivi sasa saa tatu nitoke nirande, basi huko njiani labda nitakutana na jambo gani. Unitembea kifua mbele, unakwenda kutoka hapa Dodoma mpaka Dar es Salaam bila ya wasiwasi na tunafika salama salimini Dar es Salaam na magari yanakwenda bila kuzuiliwa. Kwa hili, nalipongeza Jeshi la Polisi liendelee kufanya kazi hii kubwa sana wanayoifanya ili tupate amani na utulivu na tujitanue katika Tanzania yetu hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nazungumzia suala la ujenzi wa makazi na Vituo vya Polisi. Kwa kweli Serikali imechukua jitihada; na sasa hivi nilivyoipitia hotuba hii, inazungumzia kwamba kila mkoa utajengwa nyumba ishirini ishirini.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli sisi Mkoa wetu wa Kusini kuna nyumba pale Paje na kuna baadhi ya nyumba zile nne pale tayari zilishakuwa zinakalika na nyingine bado kidogo kupauliwa. Nasema hivi, nyumba zile ziendelee kuboreshwa ili Polisi wapate kukaa vizuri waweze kufanya kazi zao vizuri na hasa ukizingatia ukanda ule ni wa watalii. Hili nalizungumza kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, bado vituo havijakarabatiwa. Kwa Mkoa wetu wa Kusini kuna vituo baadhi tu; kuna Kituo cha Dunga tayari kiko kinajengwa, kuna Kituo cha Chwaka tayari kinafanya kazi; lakini kuna baadhi ya vituo bado havifanyi kazi vizuri, havijakarabatiwa ukaridhika Polisi wako katika mazingira mazuri juu ya vituo vile. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Polisi cha Makunduchi wameweka foundation toka 2015, foundation ile mpaka leo bado haijapata msaada wowote. Serikali haijaweza kuinyanyua ili kile kituo kiendelee kiwe cha kisasa. Bado Serikali, juu ya jitihada zake inazozichukua lakini bado haijafikia malengo hasa tunayoyataka.

Mheshimiwa Spika, nasema Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake waifanye hii kazi hasa kwa Mkoa wangu wa Kusini na huu mkoa ni mkubwa sana, maana mkoa huu ni mkoa wa watalii. Watalii wote wanapokuja Kusini Unguja, basi lazima wafike Chwaka, Paje, Makunduchi, Jambiani, kote huko kuna vikazi vyao vya kupita wakienda wakafanya utalii wao.

Mheshimiwa Spika, kuna suala la mafao ya polisi na mahitaji yao ambayo polisi wanapokuwa tayari wameshapandishwa vyeo, basi polisi anapandishwa cheo na anakaa muda mrefu bado hajapata stahiki yake inayotakiwa. Hili nimeshalizungumzia mpaka katika swali langu la msingi, nikazungumza kwamba mafao ya polisi ni bado, polisi wanalalamika mafao bado hawajayapata.
Mheshimiwa Waziri …

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Mwantumu Dau.

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja, Mheshimiwa Waziri anapokuja hapo aje atuambie kuhusu habari ya mafao ya polisi, maana alisema mpaka mwezi wa Tano itakuwa tayari hapa. Kwa hiyo, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante sana. (Makofi)