Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii, ingawaje kwa kweli haukuwa mpango wangu hasa kuongea lakini imebidi niongee kwa sababu zifuatazo.

Mheshimiwa Spika, jana nilikuwa namtania Mama Makilagi hapa aliposema haongei na watoto na mimi nikasema mimi ndiyo baba yao na Bunge likacheka kidogo. Kwa muktadha huo nataka niseme hivi, imetokea lugha hapa kwamba kambi yetu hii hatuthamini kazi ambazo zinafanywa na Jeshi la Polisi.

Mheshimiwa Spika, sasa nataka niseme kwamba hii si kweli. Nichukue fursa hii kwa niaba ya wenzangu kuwapongeza askari wote wa jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza, Jeshi la Uhamiaji, Jeshi la Zima Moto ambao wanafanya kazi yao vizuri. Rai yetu hapa ni mbili tu ya kwanza ni kulikumbusha na kuliomba Jeshi la Polisi kufanya kazi zake kwa kufuata sheria hiyo ndio rai yetu tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa hili hakuna anaweza kusema kwamba Jeshi la Polisi lifuata sheria mia kwa mia hakuna kwa sababu yapo matukio kadhaa katika nchi yetu ambayo yana-prove tofauti. Kwa mfano juzi, juzi kuna kijana alikamatwa Waziri Dhahiri pale Lembeli amekamatwa asubuhi saa mbili amepigwa na askari mpaka kafia kituoni. Sasa askari kama huyu ni moja kati maskari ambao hawafuati sheria, hawafuati taratibu na matukio kama haya yapo maeneo mengi. (Makofi)

Kwa hiyo sio sahihi kusema kwamba tunaosema Jeshi la Polisi lijirekebishe lifanye tathimni ya baadhi ya askari wake sio sawa sawa na kusema kwamba hatulipendi jeshi la polisi wala asitokee mtu akasema eti kwamba ikitokeo polisi wasiwepo kwa masaa machache itakuaje haitatokea mpaka dunia itakapokwisha.

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Taarifa Mheshimiwa Selasini pokea taarifa Mheshimiwa Chief Whip.

T A A R I F A

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa mchangiaji anaochangia nimpende kumkumbusha kwamba moja ya mambo ambayo jana yalifanya kiasi kwamba Wabunge wa Chama cha Mapinduzi wakafikia kusema kwamba hawa hawawapendi polisi wetu ni kwamba mchangiaji wao mmoja alifikia kusema kwamba polisi ni kansa ya Taifa. Nakupa taarifa kwamba hilo neno sio nzuri na tunafahamu kabisa kwanza kansa hata nikisikia kansa naogopa polisi hao hao wanaolinda usalama wetu na sisi tupo salama hapa wanapotamkwa kwamba wao ni kansa la Taifa hilo neno linaukakasi nashukuru.

SPIKA: Mheshimiwa bado Mheshimiwa Selasini kidogo. Sikupata privilege ya kulifahamu hilo lakini kama limesemwa na Mbunge ningeomba nifahamu tu wala usifiche ni Mbunge nani?

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Sophia Mwakagenda wakati anachangia jana alisema kabisa wazi na Hansard zitaeleza kwamba polisi ni kansa ya Taifa.

SPIKA: Ahsante naomba mniletee hiyo hansard sijui kama Mheshimiwa Sophia yupo lakini kama Wabunge haya ni majeshi yetu, hata uwe na chuki kiasi fani kuna mstari ambao huwezi kuvuka. Kwa hiyo, ni vizuri Chief Whip unaongea basi endelea.

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, ahsante natumai utanihifadhia muda wangu.

Mheshimiwa Spika, nilivyoanza kusema nimesema nasimama kama kiongozi wa kundi hili, na Mbunge aliyeongea angekuwa amesoma saikolojia angekuwa amesoma kitu kinaitwa furious of generation haiwezekani kauli ya mtu mmoja ikawa kauli ya wote, na Mbunge hili lina taratibu zake kama kuna mtu mmoja amezungumza Bunge hili lina namna ya kumdhibiti huyo aliyezungumza. Lakini kama kiongozi wa kundi hili nasema hatuna msimamo wowote wa kulidharau jeshi la polisi kwa namna yoyote ile na ninawapongeza polisi ambao wamekuwa wakifanya kazi vizuri full stop hakuna zaidi. (Makofi)

T A A R I F A

SPIKA: Almas Maige.

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, Msemaji wa Kambi ya Upinzani kutoka CHADEMA huko nje, huko nje amesema mambo mengi na kulikashifu Jeshi la Polisi na ndiye Msemaji wa Kambi ya Upinzani, sasa wanakanusha au wanakubali?

SPIKA: Mheshimiwa Selasini unaipokea taarifa?

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, ninampa pole rafiki yangu katika utu uzima huu alipaswa vilevile awe amezijua kanuni. Pamoja na hayo sote kwa pamoja kama Wabunge wajibu wetu ni kulisaidia Jeshi la Polisi. Tunasema kwa pamoja jeshi letu lina matatizo, askari wetu wanahitaji nyumba bora wote, wa polisi, wa magereza, wa uhamiaji hili sio suala la upinzani ni suala letu wote na kila Mbunge akisimama hapo anazungumza kuhusu nyumba za askari kwenye jimbo lake.

Mheshimiwa Spika, tunazungumza juu ya vitendea kazi vya polisi, tunazungumza habari ya vituo bora vya polisi, jeshi letu kwa sasa ni jeshi ambalo unakwenda kituoni wanahangaika na makaratasi na mafaili na kadhalika. Watu wameshaenda sasa hivi kisasa watu wana komputa na kadhalika na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunazungumza hayo, tunazungumza habari ya mishahara na posho za askari wetu. Tunazungumza habari ya uniform za askari wetu haya ndiyo mambo ya kuzungumza na Mheshimiwa Kangi Lugola Waziri ametuletea hotuba hapa tuijadili sisi kama Wabunge sio kumjadili Mheshimiwa Tundu Lissu hayumo humu kwenye hotuba ya Waziri. Kwa hiyo, wakati mwingine tunatumia muda Wabunge vibaya kugeuza kila jambo kuwa jambo la siasa wakati huu muda ni muda wa wanaotulipa mshahara, wanaotuliapa posho ambao ni wananchi wa Tanzania wanaolihitaji hili jeshi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema wako askari ambao wanalifedhehesha jeshi la polisi na ushahidi ni kwamba limekuwa likichukua hatua dhidi ya askari wa namna hiyo. Tunachosema kasi ya kuchukua hatua iendelee.

Mheshimiwa Spika, na wewe unakumbua hotuba za Mwalimu Nyerere, Mwalimu Nyerere alikwisha kusema kuna vyombo viwili tu sasa hivi tunavitegemea sana watanzania. Chombo cha kwanza ni mahakama, chombo cha pili ni polisi. Mwalimu alisema polisi na mahakama wakiingia kwenye rushwa au kutotenda haki itakuwa ni balaa. Tunazungumza habari ya mikutano hapa, kusumbuliwa hapa, pilipili usizozila haziwezi kukuwasha sisi tunazungumza kwa sababu tunajua kinachotokea lakini polisi hawa lazima wawe mfano katika kutekeleza sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati sheria ambayo wanapaswa watekeleze, polisi hawaruhusuwi kuingia kwenye active politics kwa sababu wao wanafanya maamuzi, jeshi hili ni la wote. Sasa polisi kuwa tamed na Watanzania kwamba ni la CCM na la Chadema watu wa upande mwingine hawatawapa ushirikiano na matokeo yake utendaji wa jeshi la polisi hautakuwa sawa. Kwa hiyo, ndugu zangu tunapozungumza habari ya kuriboresha jeshi la polisi hatuzungumzi kwa sababu ya chuki na jeshi la polisi. Tunazungumza kwa sababu tunalipenda na tunapenda lifanye kazi vizuri zaidi. Tunazungumza ili Waziri na Naibu wake wapate uwezo wa kulisaidia zaidi.

Mheshimiwa Spika, na mwisho pale kwangu Rombo lile ni jimbo ni jimbo la mpakani Mheshimwa Waziri angalia uwezekano wa kusaidia wale polisi ili ule mpaka uweze kufanya kazi vizuri. Na sisi watu wa Rombo tunashirikiana vizuri na Jeshi la Polisi tumejenga kituo pale Useri kwa nguvu zetu tumekabidhi Serikalini sasa hivi tuna msingi kwenye Kata ya Mahida unakwenda, tuna msingi umeshafika leta kwenye Kijiji cha Kilongo chini msingi wa kituo cha polisi na wa nyumba za polisi. Huo ni ushahidi kwamba tunasaidiana na jeshi lenyewe na Serikali katika kuliboresha.

Mheshimiwa Spika, nimalizie tu kusema kama tunatendelea na vijembee katika hoja kubwa kama hii ya jeshi tunaiweka nchi yetu katika hatari kubwa sana kwa sababu tunaligawa jeshi tugawa na wananchi. Kwa hiyo, naomba tu ni rai yangu chukueni hoja ambazo zinaweza kusaidia jeshi upande huu zichukuliwe zinaweza kuisaidi jeshi upande tuweze kujenga jeshi bora kwa ajili ya nchi yetu. Ahsante sana nakushukuru sana. (Makofi)