Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, nianze na pongezi nyingi sana kwa Waziri Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe, Naibu Waziri, Mheshimiwa Juliana Shonza na Watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuinua vipaji na kuendeleza soka la Tanzania pamoja hotuba yao iliyowasilishwa hapa Bungeni.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mambo mazuri yaliyoorodheshwa katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri, nilikuwa naomba nipatiwe ufafanuzi wa mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na ripoti nyingi sana za mchakato wa Vazi la Taifa na tumekuwa na kiu kubwa sana kuona mchakato huo unafika mwisho ili Tanzania itambulike kwa vazi lake kama zilivyo nchi nyingine. Je, ni lini sasa Serikali itahitimisha hili jambo zuri?

Mheshimiwa Spika, vijana wetu wa kike wamekuwa wakishiriki Mashindano ya Ligi (soka) Timu za Wanawake, wakiwa na changamoto nyingi sana kiasi kwamba hata ushiriki wao umekuwa mgumu. Nilitegemea ligi hii ingetumika hata kupata vipaji kwa mabinti zetu ili waweze kushiriki katika Timu ya Taifa ya wanawake.

Mheshimiwa Spika, napenda kujua mkakati wa Serikali wa kusaidia hizi Timu ziweze kushirihiki ligi kuu, kwa sababu wanaishi katika mazingira magumu mpaka wanadhalilishwa kwa kutembeza mno bakuli.

Mheshimiwa Spika, nashirikiana na wote walioipongeza TBC kwa kazi nzuri sana. Nilikuwa naiomba Serikali itoe kipaumbele kuongeza bajeti ili waboreshe mitambo, pia usikivu uwepo katika maeneo yote kuliko ilivyo sasa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.