Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, awali ya yote namshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai kwetu sote. Nampongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuona umuhimu wa Wizara hii na kumteua Waziri na Naibu Waziri walio waelewa na makini sana kwenye kazi zao.

Mheshimiwa Spika, ninampongeza Mheshimiwa Dkt. Harrison Mwakyembe na Mheshimiwa Juliana Shonza, Katibu Mkuu Ndugu Susan Mlawa, Naibu Katibu Mkuu Ndugu Nicholaus B. William, Mkurugenzi wa Habari Dkt. Ryoba na Viongozi wote Wakuu kwenye Idara nyingine ikiwemo Sanaa na Michezo.

Mheshimiwa Spika, nakubali kabisa kwamba kuna mambo ambayo yanatendeka, yanabadilisha utamaduni wetu bila hiari yetu Watanzania, kutokana na uwepo wa mitandao kama luninga, simu na kadhalika. Baadhi ya mambo hayo ni mavazi yasiyo ya heshima, maigizo ya filamu za nje na mengineyo. Je, Serikali ina mpango gani kukomesha vituko hivyo katika hatua za awali kama kwenye Shule za Msingi?

Mheshimiwa Spika, naipongeza sana Idara ya Habari. Tatizo langu ni mtiririko wa taarifa ya habari asubuhi. Je, ni lini TBC itatangaza habari mfululizo bila kuingiliwa na majadiliano yoyote ili tuwahi kazini?

Mheshimiwa Spika, kuhusu michezo. Inaumiza sana kuona jinsi ambavyo hatujaweza kuingia kwenye kiwango cha juu cha Kimataifa kwenye soka. Nataka ieleweke kuwa, maandalizi yetu ya zimamoto hayatatufikisha mbali. Kila Wizara iwe na dawati la michezo mahali pa kazi.

Mheshimiwa Spika, napendekeza wachezaji waandaliwe toka utotoni kwa lishe bora, elimu na mazoezi. Makuzi ya wanamichezo yasimamiwe toka awali na wazazi na waalimu.

Mheshimiwa Spika, mwisho, naunga mkono hoja na ninaomba kwenye miaka ijayo waongezewe fedha zaidi bila ukomo.