Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nimpongeze Waziri pamoja na timu yake kwa kazi kubwa wanayoifanya.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Lushoto ina wasanii wengi mno, lakini wasanii wale hawajulikani kwenye tasnia ya vyombo vya habari na ukiangalia Serikali pamoja na kupoteza mapato mengi ya kuchangia Taifa letu unakuta tunazikosa, lakini pia wasanii hawa kupoteza taaluma yao na mwishowe hujiingiza kwenye mambo ambayo hawana fani nayo na kupoteza mwelekeo wa maisha yao. Kwa hiyo niishauri Serikali yangu tuwawekee miundombinu rafiki ili tusipoteze vipaji vya wasanii hawa kwani mwisho wa siku Taifa letu litaongeza mapato kupitia wasanii wetu hasa wasanii wa Lushoto.

Mheshimiwa Spika, pia Wilaya ya Lushoto ina vijana wengi wana vipaji vya mchezo hasa mpira wa mguu, lakini pia kuna changamoto kubwa ya kiwanja cha mchezo. Kwa hiyo, niiombe Serikali yangu Tukufu itujengee uwanja wa michezo katika Jimbo la Lushoto ili tuweze kuwapata kina Mesi kutoka Lushoto. Pamoja na hayo niishauri Serikali yangu hasa Waziri mwenye dhamana, michezo ifundishwe mashuleni ili kubaini vipaji toka mashuleni.

Mheshimiwa Spika, najua upo UMISHUMTA na UMISETA, hii haitoshi, kuwe na ratiba ya vipindi katika shule zetu. Pia, niiombe Serikali yangu hasa Waziri mwenye dhamana wakati wanawatafuta wachezaji hasa hawa wa chini ya miaka 17 waende mpaka wilayani kwani kuna wachezaji wazuri mno wanakosa tu kuonekana katika vyombo au hakuna wa kuwasemea.

Mheshimiwa Spika, Redio ya Taifa ni shida katika Wilaya ya Lushoto. Kwa hiyo, niiombe Serikali yangu itujengee mnara wa TBC 2 ili wananchi wa Lushoto waweze kupata mawasiliano ya matangazo ya habari kuliko ilivyokuwa sasa. Booster imefungwa kwenye mnara wa redio, kwa hiyo kusababisha usikivu wa TBC kuwa mdogo yaani usikivu hauendi mbali na kama tunavyojua TBC ndio redio yenye uhakika wa taarifa zake.

Mheshimiwa Spika, mwisho, nisisitize kuwekewa mnara wa TBC ni muhimu mno hasa kwa maslahi ya wananchi wa Lushoto.