Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa fursa hii na nampongeza sana mtoa hoja, Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri na wasilisho lililojaa weledi wa hali ya juu.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuipongeza Timu yetu ya Taifa kwa kuweka historia ya kufuzu Mashindano ya Mataifa ya Afrika maarufu kama AFCON yatakayofanyika nchini Misri Juni, 2019. Ni matumaini yangu na Watanzania baada ya kusubiri kwa miaka 39, TTF watajipanga vilivyo katika kuandaa timu yetu ili iweze kufanya vizuri katika mashindano hayo.

Mheshimiwa Spika, usimamizi wa viwanja vyetu hususan vya kuchezea soka uangaliwe kwa karibu na mamlaka husika. Kwa mfano, kwenye mashindano ya ligi kuu viwanja vingi hususan vya mikoani vipo katika hali mbaya kiasi kiasi cha kuhatarisha usalama wa wachezaji wenyewe. Naomba wasimamizi wa mpira nchini (TFF) waweke utaratibu madhubuti timu zinazocheza katika ligi kuu viwanja vyao vikaguliwe na wasiokidhi viwango walazimishwe kucheza kwenye viwanja vya jirani vyenye ubora.

Mheshimiwa Spika, Tanzania ilikuwa inasifika duniani kwenye mchezo wa riadha. Siyo siri wanariadha hawa wengi chimbuko lao lilikuwa Wilayani Mbulu, Mkoani Manyara. Umefika wakati sasa Wizara ikaona haja na hoja ya kujenga Chuo cha Michezo Wilayani Mbulu ili kulea vipaji vya vijana ili wengi wapate fursa.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru na naunga mkono hoja.