Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, kwa nini timu ya hamasa ya kui-support timu ya Taifa iliundwa na Wanasiasa, Mwenyekiti wake akiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam? Suala hili linagawa watu kwa kuwa siyo watu wote ni wana CCM. Binafsi sikuunga mkono kwani ilikuwa movement za kisiasa, tuache kuingiza timu zetu katika siasa, uzalendo siyo kampeni ni hiari ya watu kupenda nchi yao. Hii ni aina nyingine ya siasa kwenye Wizara hii, wote tunajua mchakato na sababu za uzalendo.

Mheshimiwa Spika, upungufu katika Sheria ya Huduma za Habari kama ilivyothibitisha Mahakama ya Afrika Mashariki (EAC), sheria hii irudishwe mara moja na kufanyiwa marekebisho.

Mheshimiwa Spika, TBC kuendelea kutumika kama chombo cha propaganda cha CCM. Ni aibu sana kwa Nchi yetu. Rejea vipindi mbalimbali kwenye TBC, swali, je, hii ni TV ya Chama? Mbona kazi za vyama vingine hazionyeshwi? Kuweni wazalendo tuondoe aibu hii kwa Taifa.

Mheshimiwa Spika, ni lini Bunge litaanza kuoneshwa live. Niishauri Wizara kuja na mapendekezo ya kurudisha live broadcasting kwa kuwa ni pesa ya wapigakura. Je, ni sahihi kuwanyima haki ya kujua kinachojadiliwa na kuamuliwa na wawakilishi wao?

Mheshimiwa Spika, maandalizi ya Olympic; nashauri tuwaandae vijana katika michezo mingine kama kurusha tufe, mishale na hata kuruka kwa kuwa tumeshindwa kufanya vizuri katika mpira na kukimbia, hivyo hatuna budi kuangalia nyanja nyingine.