Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Spika, natoa shukrani na pongezi za dhati kwa Rais kutokana na utekelezaji wake kwa maendeleo ya nchi kwa wananchi wake. Jinsi anavyowasimamia na kuwaelekeza wasaidizi wake katika kutimiza majukumu yao kwa mafanikio ya wananchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, nawapongeza Waziri na Naibu Waziri bila kuwasahau Katibu Mkuu na wataalam wote ndani ya Wizara kwa kusimama na kutekeleza majukumu yao na kutuwezesha wananchi na wadau wapenda michezo utamaduni na sanaa kufarijika na kuwa na matumaini makubwa kwa kusonga mbele na michezo, sanaa na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa ushauri kwamba inasikitisha kila vijana wanapojitahidi kufanya vizuri wanaishia kwenye robo fainali. Naomba nasi tuwachukue vijana wetu kipindi chote na haya mazoezi ya kila siku kama ajira kwao, hadi mashindano yawakute humo humo, kuliko tunavyofanya mazoezi ya matukio, ni kazi ngumu ndiyo maana tunaishia mahali duni. Hivyo tubuni kitu cha kuzalisha ili tupate mapato ya kuwalipa kila mwezi hawa wachezaji ili wafanye mazoezi ya kuleta ushindi kwa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, tunaomba chuo cha kuandaa wataalam wa michezo, sanaa na utamaduni kuboreshwa na kuongezewa wigo ili tupate uelewa zaidi ya kiwango cha juu, tunahitaji nasi Tanzania tuwe mfano ulimwenguni.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la wacheza sanaa wa upande wa watoto wa kike, mavazi yao hayana maadili mema. Ni vema uwepo utaratibu wa kufunika miili yao kuanzia kifua hadi chini ya magoti yao na wakacheza vizuri tu. Kwa mfano wanaume wanacheza vizuri na wakati mwingine zaidi ya wa kike huku wakiwa wamevaa kamilifu. Tunaomba sasa wakati umefika turekebishe sheria, kanuni na taratibu zitakiwavyo kuhusu mavazi ya watoto wa kike yatumikayo kwenye nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, tunaomba uwepo utaratibu kwa wachezaji wasanii na utamaduni kuwekewa bima ya afya. Pia uwepo utaratibu wa kuwaelimisha kila mara, waepukane na utumiaji wa madawa ya kulevya. Tunapendekeza tunapohitaji kutoa zawadi kwa vijana wetu ni vema tukaendeleza zawadi ya Rais aliyotoa hivi karibuni ya viwanja na hatimaye tuweze hata kuwajengea nyumba za bei nafuu kuliko pesa hatimaye wanakimbilia kununua vitu vya anasa, visivyo na faida baadaye.

Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja.