Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nilimsikiliza Mheshimiwa Waziri wakati anawasilisha taarifa yake, alisema kwamba kwa sasa tuna magazeti 216 na redio 163. Hoja si wingi wa kuwa na media nyingi. Hoja, media hizi zinafanya kazi kwa uhuru au ndiyo zile ambazo Waziri akiamuka asubuhi anafungia kwa sababu tu hazijaandika habari nzuri za kumpendeza mwenye nchi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Habari Maelezo hivi sasa imegeuka kama ni kitanzi kwa Waandishi wa Habari. Kazi kubwa ya habari maelezo sasa hivi, ukienda katika News Media zote, utakuta kuna mafaili ya maonyo ya kuwaambia kwa nini wasifutiwe, ya kujieleza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, habari maelezo badala ya kuwaelekeza vyombo vya habari vifanye nini, Wahariri wafanye nini, sasa hivi imegeuka kama kitanzi kwa ajili ya kuhakikisha inafungia magazeti yoyoteyale ambayo hayaandiki habari nzuri ambazo zinaipendeza Serikali, badala yake yanahangaika na magazeti ambayo yanaandika habari za kuikosoa Serikali hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, CAG alizungumza na Media, kama haitoshi, Mwenyekiti ACT naye akaitisha media kwa lengo la kuchambua taarifa ya CAG, Dkt. Abasi, anawaandikia wahariri ambao waliandika habari ambazo ni za uchambuzi zilizofanywa na chama cha ACT. Haki iko wapi, CAG ambaye ndiye aliyekuwa chanzo cha taarifa hizo, asichukuliwe hatua, lakini kwa sababu Zitto ametoa ufafanunzi na waandishi wameandika, basi vyombo hivyo havina mamlaka, vinataka kufungiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hatuwezi kuendesha nchi kwa nama hii. Maana yake ni nini, kwamba sasa hata vyama vya upinzani, visifanye press, maana yake ni hiyo kwa sababu kama umepewa onyo usifanye press za upinzani, maana yake ni kwamba tunataka kuvinyima uhuru vyombo vya habari vifanye kazi za kuchagua, zifanye kazi za Serikali tu peke yake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama kulikuwa kuna defamation yoyote, ilipaswa, kabisa, angewajibika Zitto na si vyombo vya habari! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ajili ya muda, suala la Bunge Live, tuliambiwa Bunge Live hatuonyeshi kwa sababu wananchi wako busy kufanya kazi. Sasa hivi Rais anafanya ziara, ziko live, je, hao wananchi sasa hivi hawafanyi kazi! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapoyazungumza haya, tunataka kuangalia upande mwingine wa shilingi, lakini kama haitoshi, hata hapa Bungeni tulipo, tukichangia chochote hapa, kinakatwa! Wakati mwingine clips za Wabunge hazitolewi kwa wandishi, kwa nini? Tunaogopa nini! Hili Bunge ni huru tumekuja kwa ajili ya kuwawakilisha wananchi, taarifa zinazoandikwa kwa maandishi hazikatwi, lakini ikifika kwenye jambo ambalo tunaikosoa Serikali, clip haitaonekana! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna haja gani ya kuendelea kuwa na Bunge ambalo, tuna haja gani ya kuendelea kuwa na waandishi ambao wanafanya kazi ya Bunge hapa ambao mwishoni clips zote zinafutwa, hakuna kazi iliyofanyika. Hili halikubaliki na tunasema kwa masikitiko makubwa, tuna haki ya kupewa kile tulichochangia hapa. Kama ilivyo upande wa CCM wanapewa na sisi Upinzani tuna haki ya kupewa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukizungumza kuhusu kufungiwa kwa magazeti, sijui Waziri anatoa wapi mamlaka ya kufungua magazeti. Kwa mujibu wa Sheria ya Habari tuliyoipitisha 2016, hakuna sehemu ambayo inamtaka waziri kufunga magazeti. Anapofanya kosa Mwandishi kama Mwandishi, anawajibika yeye, unapokifungia chombo, kuna wafanyakazi wengine, kuna madereva, kuna wahudumu, kuna watu wengine Waandishi, wanawajibika kwa kosa la moja mmoja, si sawa! Haya ndiyo mambo ambayo tunasema Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha atueleze. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)