Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nipongeze kazi kubwa inayofanywa na Wizara hii chini ya Waziri Mheshimiwa Dkt. Augustine Philip Mahiga, naishauri Serikali iwajengee nyumba maalum Majaji na Mahakimu kutokana na kazi zao za kusimamia sheria na maslahi mbalimbali na waweze kuwa na ulinzi wa kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wizara hii ikamilishe upelelezi wa kesi kwa wakati ili kupunguza msongamano wa watuhumiwa magerezani na mahabusu. Fedha zinazotolewa za bajeti zipelekwe kwa wakati ili kutekeleza na kukamilisha miradi ya maendeleo kwa wakati. Pia naishauri Serikali ikarabati Mahakama za Mwanzo hadi Wilaya, mfano, Mahakama ya Mwanzo ya Temeke Dar es Salaam ni chakavu na ndogo haikidhi mahitaji; Serikali iongeze vyuo vya mafunzo ya Mahakama ili kuweza kupata wataalamu wa sheria wa kutosha.