Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu umuhimu wa marekebisho ya Katiba kwa ajili ya kupata Tume Huru ya Uchaguzi, kwa nini wanasiasa wanatakiwa kuwa Wakurugenzi wakati ni returning officer wa chaguzi za Jimbo? Mfano, Mhagama aliyekuwa Katibu wa CCM Mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mlundikano wa maabusu wakati kesi zao zinadhaminika ilihali wanatumia fedha za Umma katika kuwa-sustain, kumekuwepo na ucheleweshwaji mkubwa wa kesi kunakosababishwa na Ofisi ya Taifa ya DPP, Mwendesha Mashtaka, kwani maelezo ya Polisi mara zote yamekuwa, file bado liko kwa DPP.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kurejeshwa haraka kwa mchakato wa Katiba mpya, ufanyike mara moja kwani Katiba zilizopo zinaonesha upungufu mkubwa na imeendelea kupigiwa kelele. Vile vile sheria ya maudhui ya mtandao inaonesha nia mbaya ya Serikali ya Awamu ya Tano katika kutoa maoni na uhuru wa kujieleza licha ya kuwa na vifungu vinavyokiuka mikataba ya Kitaifa. Hivyo ifutwe mara moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Serikali kujikita kwenye sensorship ya vyombo vya habari hasa magazeti kupitia Msemaji Mkuu wa Serikali, hii ni kulitia aibu Taifa na kuonesha ubeberu wa kiutawala.