Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kuna malalamiko ya wananchi kuhusu uvunjifu wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu masuala ya haki za wanawake, watoto na walemavu; nashauri Serikali ijipange kuyachunguza maeneo haya ili uvunjifu huu uishe. Wanawake wananyanyasika sana, hususan katika jamii na Magerezani. Ni kwa nini Serikali hii ya Awamu ya Tano imeshindwa kumaliza malalamiko haya ambayo kila siku yanaongezeka kupitia vituoni, Polisi na Mahakamani? Hii inasababisha kuteseka kwa wanawake na watoto ambao kimsingi ni kundi kubw. Hivyo Serikali iondoe malalamiko haya mapema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mlundikano wa mahabusu Magerezani na Vituo vya Polisi, mamlaka inayoshughulikia masuala haya imeshindwa kumaliza jambo hili. Gereza la Kalika, Nkulunkulu lililopo Mpanda mpaka leo mahabusu na wafungwa wanafanyiwa vitendo viovu na Askari Magereza na hawana sehemu ya kulalamika wakihofia maisha yao, kwa sababu hawa Askari wanaishi nao. Wanapoumwa hawashughulikiwi vya kutosha na kusababisha afya zao kuwa duni na ukizingatia wanalundikana katika Magereza hayo ambayo kiafya inakiuka haki za kimsingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili, Serikali imeshindwa kutatua kwa sababu malalamiko bado yanaongezeka. Je, Serikali haioni kwa kushindwa mambo haya inafanya makusudi kupoteza nguvukazi hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni vita dhidi ya rushwa. Matatizo ya kiuhalifu yataendelea kuongezeka kwa sababu baadhi ya Askari wasio waaminifu wamekuwa wakipokea rushwa na kuwaacha walalamikaji wakiishi katika maisha ya wasiwasi. Mahakama na Polisi ikishindwa kudhibiti mianya ya rushwa na tunaamini katika vyombo vya sheria ndiyo sehemu pekee inayoweza kutafsiri makosa, hii inaleta tafsiri mbaya katika jamii na wananchi wataamua kujichukulia hatua mkononi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni ukarabati wa majengo ya Mahakama za Wilaya na Miko. Bado hali ni mbaya na hairidhishi katika Mahakama zetu. Uhifadhi wa mafaili ya kesi hupotea; hii inaleta picha mbaya kwamba na Mahakama zetu zinashindwa kulipa kipaumbele jambo hili.