Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia hoja hii kwa kuanza na Mahakama. Mahakama nyingi zimechoka hapa nchini hasa Mahakama zilizoko vijijini, hazina vyoo, vitendea kazi, samani na vinginevyo. Hata Mahakimu wakitoa hukumu, upatikanaji wa hati unakuwa mgumu kwa kuwa ni vigumu kupata hati au hukumu ya kesi iliyochapishwa kwa kukosa vifaa. Nashauri Serikali izingatie hilo hasa katika mkoa wangu wa Iringa kwa zile Mahakama za ngazi ya chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nyumba za Mahakimu ni chache, hii inahatarisha usalama wao, kwani wengi wao wanaishi uraiani, mitaani na wamepata usumbufu. Serikali ihakikishe inajenga nyumba za Mahakimu. Mahakama nyingi hazina mahabusu na kunapotokea wahusika kupelekwa Mahakamani inakuwa ni gharama pia kwa kuwa hawana sehemu ya kuhifadhi mahabusu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mishahara ya Mahakimu na posho kama vile posho ya nyumba lakini waendesha mashtaka wanapewa posho, hivyo na Mahakimu wapewe pia posho. Mfumo wa mashtaka ni mbovu, wananchi wengi wanaonewa sana, haki haitendeki. Nashauri mfumo huu ufumuliwe na uundwe upya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia uchunguzi unachukua muda mrefu sana.