Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitazungumzia kuhusu watu kuteswa wanapokamatwa na na Polisi kabla Mahakama haijasema kama mtu huyo ana kesi ya kujibu au la. Je, nikifungu gani cha sheria kinachompa Askari Polisi haki ya kumpiga mtuhumiwa na kumtesa kabla ya Mahakama kuamua?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la kubambikiziwa kesi. Hivi sasa kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi kuwa wanabambikiziwa kesi na hawapelekwi Mahakamani kwa wakati. Je, kwa kufanya hivi siyo kuvunja sheria?

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kuna changamoto kubwa katika ujenzi waMahakama katika Wilaya mbalimbali nchini. Jambo hili linapelekea wananchi wengi kuanza kutumikia kifungo kabla ya kufikishwa Mahakamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haki ya kupata taarifa. Sheria iliyotungwa imepelekea maumivu makali kwaWatanzania. Kupata habari/taarifa ni haki yao ya msingi wakati wote watakaohitaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndoa za utotoni. Sheria inayoruhusu ndoa za utotoni imekuwa kandamizi kwa wananchi wa Tanzania kwani kwa kiasi kikubwa kwa sasa inatumika vibaya kukandamiza watoto wa kike na kuzima ndoto zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni juu ya mikataba mibovu tunayoingia. Suala hili la kuingia mikataba mibovu inapelekea Taifa kuingia kwenye hasara kubwa na kupelekea umaskini kwa uzembe kwa kutopitia mikataba hii vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulinzi wa Mahakimu kuanzia Mahakama ya Mwanzo. Kulingana na kazi wanazofanya za kuhukumu watu ni vyema jambo hili likaangaliwa upya kwani watu hawa wanahitaji ulinzi wakiwa kazini na nje ya kazi.