Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri lakini niwapongeze Katibu Mkuu na viongozi wote wa Wizara hii.

Mheshiimiwa Mwenyekiti, nipongeze Serikali kwa jitihada kubwa za uamuzi wa kujengaMahakama Kuu na Mahakama za Wilaya maeneo ambayo hayakuwa na Mahakama. Napenda kujua ni lini Mahakama ya Wilaya ya Kilindi itakamilika maana toka msingi ukamilike, mkandarasi ameondoka site.Napata maswali mengi kwa wananchi wa Kilindi kwamba ni lini Mahakama hiyo itakamilika? Wameisubiri Mahakama hii kwa muda mrefu sana. Natumai Mheshimiwa Waziri nitapata majibu ya swali hili ili nikawajibu wananchi wa Kilindi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni ushauri kwa Wizara hii, tumeshuhudia baadhi ya miradi imesimama mfano Shirika la NHC, wakandarasi wapo site na gharama zinaendelea kuongezeka. Ili Serikali isije kuingia kwenye migogoro na kulipa gharama za kumweka mkandarasi site kwanini Wizara isifuatilie miradi yote ambayo siku za usoni inaweza kuileta Serikali hasara zisizokuwa za lazima kwa kuangilia mikataba yote ambayo haijakaa sawa?Tumeshudia haya kwenye maeneo ya barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.