Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Nkasi ina umri wa miaka 40 lakini Makao Makuu ya Wilaya Namanyere haina jengo la Mahakama ya Wilaya wala Mahakama ya Mwanzo. Cha ajabu sana kila mwaka hotuba ya Waziri utakuta Namanyere watajenga jengo la Mahakama lakini mwaka huu hakuna kitu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ajabu sana Makao Makuu ya Wilaya hakuna jengo la Mahakama ya Mwanzo wala ya Wilaya wakati wilaya mpya zimepewa fedha za majengo ya Mahakama ya Wilaya, hii si haki kwa Wilaya ya Nkasi. Wilaya ya Nkazi tunahitaji jengo la Mahakama kama Wizara iliyoadidi kwenye bajeti ya mwaka 2017/2018 na 2018/2019.