Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Mbozi lenye vijiji 63 na kata 11 lina Mahakama mbili tu za Mwanzo. Naomba kwa niaba ya Wananchi wa Mbozi Serikali iweze kukarabati jengo la Kijiji cha Igamba, Jimbo la Mbozi ili lianze kutumika. Miaka ya nyuma jengo hili lilitumika kama Mahakama ya Mwanzo, Igamba. Jengo hili likikarabatiwa litafanya Jimbo la Mbozi kuwa na Mahakama tatu za Mwanzo za Itaka, Mlowo na Igamba. Hivyo, ni vema Serikali ikawasaidia wananchi wa Igamba ili kuwaepusha na safari ndefu ya kwenda kutafuta huduma hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, Mahakama ya Mwanzo Itaka licha ya kwamba inatumika lakini imechakaa sana hivyo, Serikali ichukue hatua za haraka ili kulinusuru jengo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakama ya Wilaya Mbozi iliyopo Mji wa Vwawa ipo katika hali mbaya sana. Ukumbi wa Mahakama ni mdogo sana na miundombinu mbalimbali kama vile vyoo vipo katika hali mbaya sana. Mahakama ya Wilaya ya Mbozi kwa sasa ndiyo Mahakama ya Mkoa wa Songwe. Naishauri Serikali ikarabati Mahakama hiiili iweze kuwahudumia wananchi wa Mkoa wa Songwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, Mahakimu waongezwe mishahara ili wafanye kazi wakiwa na ari nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.