Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. PETER A. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 4 Machi, 2019, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa Ikulu alizungumza sakata la Mo Dewji na akasema anashangazwa na namna ambavyo polisi wameshughulikia. Pia akasema kabisa Watanzania sio wajinga, picha iliyochezwa haiingii akilini; ni maneno ya Mheshimiwa Rais. Mheshimiwa IGP akasema ndani ya siku nne atatoa taarifa, atasema kinagaubaga nini kilichotokea, leo ni siku ya 42, IGP kachuna, kakaa kimya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Azory Gwanda amepotea, ama amepotezwa hatufahamu, hayupo duniani ama sijui yupo wapi hatujui. Mheshimiwa Lissu kapigwa risasi mchana kweupe, Ben Saanane mpaka leo hajulikani yupo wapi. Watu wameokotwa kwenye mifuko ya sandarusi kwenye fukwe za bahari ya nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia maneno ya Rais aliyomwambia IGP na akasema Watanzania sio wajinga, kwenye kitu ambacho kilikuwa wazi, ambacho hakijajificha cha Mo Dewji, Rais akasema hapa haiko sawa na IGP akasema kwamba hili ndani ya siku nne nitalishughulikia, hivi kama hivi imefanyika kwa Mo Dewji, jambo lipo wazi kiasi hiki, hawa akina Mheshimiwa Lissu, hali ikoje, akina Ben Saanane, watu wa kawaida hali ikoje? Ni mambo mangapi yanafanyika katika nchi hii kwa taswira hii ambayo watu hawapo accountable kwa hayo mambo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza jambo hili ni fedheha, kitendo cha IGP kutamka hadharani atatoa majibu ndani ya siku nne halafu mpaka leo amekaa kimya na Serikali wamekaa kimya, jambo zito kama hili, hii inamaanisha kabisa kwamba nchi yetu haina utawala wa kisheria. Hii inamaanisha kabisa kwamba Serikali ya CCM hawawajibiki kulinda raia wa Tanzania; ni mfano wa dhahiri kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hivyo ndivyo jinsi ilivyo, naomba iundwe tume maalum ya kufuatilia mambo yote haya na tume hii iwe na hadhi ya kimahakama. Kama Rais anaweza akatoa jambo na akasema Watanzania wana akili, wameona kuna matatizo na IGP akasema ni kweli ndani ya siku nne nitatoa maelezo, leo siku ya 42 amekaa kimya, maana yake kuna mambo mengi katika nchi hii hayapo sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kabisa tume ikiundwa yenye nguvu ya kimahakama, ipitie mambo yote; ipitie jambo la Ben Saanane, Azory Gwanda, Akwilina na Mheshimiwa Lissu. Mambo yote haya yaje na ikiwezekana hii tume ije iripoti Bungeni ili Wabunge tuweze kusema way forward nini kifanyike kwenye nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna Sheria ya Uhujumu Uchumi na Utakatishaji wa Fedha. Hii sheria inawezekana kabisa iliundwa kwa nia njema kabisa lakini kwa jinsi ambavyo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)