Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia fursa hii ya kuchangia na ningependa zaidi kujikita katika suala la mrundikano wa mahabusu ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa takwimu ambazo zipo ndani ya nchi yetu, kwa hali ya magereza ni kwamba katika watu wote ambao wapo magereza/mahabusu ni asilimia 53.3. Pamoja na hayo pia tuna sheria ndani ya nchi hii ambazo ni kandamizi na zenyewe pia zinachangia kuongeza idadi ya mahabusu hao ndani ya magereza yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano ni Sheria ya Money Laundering na hizi za Uhujumu Uchumi ambazo zimewekwa na hazimpatii mtuhumiwa dhamana anapokuwa amekwishashtakiwa. Sasa suala linalokuja ni kwamba, sheria hii sasa inatumika kuweza kuwaonea na kukandamiza watu na inawezekana hata baadaye ikatumika hata kuwaumiza watu kisiasa kwa sababu namna bora ya kuwaondoa watu katika maeneo ya nchi yao na kuwa huru ni kumpa mtu kesi ya money laundering. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona mfano wa kesi ambazo zinaendelea, kesi inaendelea kwa miaka minne, miaka mitano hakuna usikilizwaji wa msingi unaoendelea hata upelelezi wenyewe haujakamilika. Sasa umempeleka mtu mahakamani kwa sababu gani kama upelelezi haujakamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme tu kwamba tunahitaji kuwa na utashi wa kisiasa kati ya Ofisi ya DPP, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na mahakama zetu ili hatimaye kuweza kuondoa hili tatizo. Kwa hilo, naiomba Serikali sasa iweze kuleta mabadiliko ndani ya Bunge hili, tuweze kubadilisha sheria hizo za Money Laundering ili tuache kuwaonea Watanzania, tuache kuwaonea watu ambao wanafanya kazi zao ndani ya nchi hii, kama mtu ana kesi, basi tutafute namna bora ya lawama hizi zisiweze kuendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namna bora ambayo nadhani inaweza ikasaidia ni pamoja na kuwa na muda maalum wa kesi hizi kufanyika, hakuna muda ambao umewekwa kisheria. Tuwe na mfano, kama sheria zile za uchaguzi ambazo zina muda maalum kwamba kesi hii iishe ndani ya muda Fulani. Kwa hiyo kama kesi humpi mtu dhamana, angalau basi uweke kwamba itakwisha ndani ya miaka miwili au mitatu, huyo mtu awe ameshaondoka na tatizo hilo liishe, kama mtu anafungwa ama kama mtu huyo anaachiwa huru. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia niweze kuchangia katika suala linalotuhusu sisi Wabunge wa Viti Maalum. Wabunge wa Viti Maalum tupo ndani ya Bunge kulingana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 66. Hata hivyo, kuna kitu kibaya ambacho kinaendelea ndani ya nchi hii, kilianza ndani ya Bunge hili Tukufu lakini na viongozi wengi wanaokaa ndani ya Meza wamekuwa ni watu ambao wanakemea tabia hiyo ya kipuuzi, naomba niite hivyo, lakini sasa tabia hiyo inaendelea huko nje ambapo Mheshimiwa Humphrey Polepole, Katibu Mwenezi wa CCM, amesimama na kusema Wabunge wa Viti Maalum wa CHADEMA wanapatikana mpaka wapitiwe na Mwenyekiti wao. Sasa ifike mahali tutambue kwamba huo ni udhalilishaji ambao hauruhusiwi hata na sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Polepole amekuwa anafanya kazi kwenye asasi za Kiserikali kwa muda mrefu, sasa kama hatambui haki hizo za kimsingi ambazo zinatolewa hata na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni aibu kwa Chama cha Mapinduzi kuwa na Mwenezi anayedhalilisha wanawake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na hilo naiomba…

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo…

MWENYEKITI: Ehe, hebu subiri, taarifa Mheshimiwa.

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpa taarifa mzungumzaji kwamba amesema Katibu Mwenezi wa Chama, Humphrey Polepole ametamka kwamba Wabunge wa Viti Maalum wa CHADEMA wanapitiwa na Mwenyekiti wao. Sasa neno kupitiwa hatujaelewa labda atoe ufafanuzi.

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu ambacho naomba niseme ni kwamba ifike mahali nafasi za watu na vyeo walivyonavyo viheshimiwe. Ni aibu kwa kiongozi wa nchi hii kusimama na kusema kwamba mafanikio ya mwanamke ya kisiasa yanatokana na shughuli za kingono. Tunawajengea watoto wetu fikra mbaya ndani ya vichwa vyao kwamba hakuna tena jitihada, jibu pekee ni waende wakalalane na watu huko watapata nafasi. Sasa hatuwezi tukaruhusu kuwa na viongozi wa namna hiyo. Kitu ninachokiomba sasa ifike mahali tuiombe Wizara na Serikali utaratibu halisi wa upatikanaji wa Viti Maalum ujulikane. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo, huu uchungu unaokuja sasa unajengeka na matusi ya namna hii…

MBUNGE FULANI: Taarifa.

MHE. UPENDO F. PENEZA: …ifahamike kwamba sasa tunahitaji mabadiliko ya Katiba kwa ajili tu…

MBUNGE FULANI: Taarifa ya ufafanuzi.

MWENYEKITI: Sitaki taarifa sasa.

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba tunahitaji pia mabadiliko ya Katiba ya nchi hii kwa ajili pia ya heshima ya mwanamke. Sasa ifike wakati Katiba iandike kwamba wanawake wakagombee, hata kama ni viti vya wanawake.

Mfano nchini Uganda, kuna viti vya wanawake lakini wanapigiwa kura na wananchi, inayotoa hata nafasi ya accountability, wananchi kuweza kumwajibisha Mbunge ambaye analipwa kwa kodi zao na Mfuko wa Jimbo wanapewa lakini… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)