Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kuipongeza Wizara kuona umuhimu wa mazingira na afya kwa wananchi kwa kutoa tamko la kusitisha matumizi ya mifuko ya plasitikic kuanzia tarehe 1 Juni, 2019. Kama tujuwavyo, mazingira bora na usafi ni kiunganishi kikubwa cha kuondoa umasikini na kukuza uchumi wa nchi na kuleta maendeleo kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jamii ni lazima ihamasishwe kuwa rafiki wa mazingira na waelimishwe kuwa uharibifu wa mazingira ndiyo unaopelekea kuharibika kwa miundombinu, upungufu wa maji, matatizo ya kiafya, upungufu wa mazao kutokana na uharibifu wa rutuba katika udongo. Vile vile kukosekana kwa mvua na ongezeko la joto vyote hivyo vinachangiwa na uharibifu wa mazingira hayo. Elimu ya kutosha kwa wananchi ni lazima iendelee kutolewa kwa kasi ili wajue umuhimu wa kutunza mazingira. Maana ukiangalia vijijini suala hili la elimu ya mazingira bado sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna changamoto nyingine ya wazoa taka mitaani. Unapomwambia Mtanzania wa kawaida, yaani mwenye maisha duni atoe shilingi 5,000/= ili taka zake zibebwe kila wiki, hapa suala la utunzaji wa mazingira tunaweza kulifanya kuwa gumu. Serikali iangalie inafanya nini katika hili ili kila mtu aweze kumudu kutoa taka kila wiki (gharama za wazoaji taka).

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia suala la mitaro katika mitaa yetu; watu wamekuwa wakikamatwa kwa kumwaga maji nje ya nyumba zao na wakati mwingine kutozwa faini hadi shilingi 50,000/= ili mradi tu pakiwa pabichi hata kama ni maji safi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kutunza mazingira na kuweka urahisi na amani kwa wananchi ili wawe rafiki na mazingira yao, Serikali iwatengezee mazingira mazuri ya kuyatunza. Kama hilo la kuwa na mitaro mitaani, tozo ya shilingi 5,000/= kwa wanaomwaga maji ovyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kusikiliza hotuba hii, pia nimeona upungufu kwa sehemu kubwa ya hotuba kugusa mazingira kuliko Muungano na hiyo kupelekea kuziacha changamoto nyingi za Muungano bila majibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile Serikali iangalie uwezekano wa kupeleka elimu ya Muungano kwenye vyombo vya habari ili watu wengi wajifunze na kupata majibu ya maswali waliyonayo, ikibidi elimu hii ianzie Shule za Msingi, watoto wakue na uelewa wa Muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia changamoto zinazokua addressed zipatiwe ufumbuzi ili tuudumishe Muungano wetu na kuondoa malalamiko yanayokuwa yanajirudia rudia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.