Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia katika hoja hii, kama ifuatavyo. Kwanza, ni matumizi ya mifuko ya plasitiki. Baada ya katazo la mifuko ya plasitiki, naomba Serikali itoe njia mbadala ya mifuko hii ya plasitiki. Serikali itoe maelekezo ya vifaa vitakavyotumika badala ya plasitiki. Mfano, vitengenezwe vifungashio kwa kutumia karatasi za kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa kuna ukataji mkubwa sana wa miti kwa ajili ya kuni na mkaa. Niombe Serikali ipunguze bei ya gesi ili wananchi waweze kutumia gesi badala ya kuni na mkaa ambao unasababisha uharibifu wa mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, masuala ya Muungano, naomba wananchi waendelee kupata elimu juu ya Muungano huu. Hata wanafunzi wafundishwe masuala ya Muungano ili kuendelea kuenzi juhudi za waasisi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.