Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na wafanyakazi wote kwa kazi wanazozifanya, hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Urambo ina Mto Ugalla. Mto huu ni muhimu sana kwa uhai wa wananchi lakini pia uhai wa Mto Malagalasi ambao unapata maji kutoka Mto Ugalla. Serikali ina mpango gani wa kuondoa magugu yaliyovamia Mto Ugalla?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya wananchi wa Urambo, naomba Serikali yetu isome tena barua rasmi iliyotumwa Wizarani kuhusu magugu yaliyovamia Mto Ugalla na kuchukua hatua za kuokoa mto huo haraka iwezekanavyo. Aidha, tunaomba semina za kuelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira na kuacha kukata miti hovyo.