Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ANTHONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Watendaji wote katika Wizara hii kwa kazi wanazozifanya katika mazingira mazuri kutokana na kutokuwa na rasilimali za kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mazingira ni suala la kufa na kupona kutokana na umuhimu wake kwa viumbe vyote duniani ikiwa ni pamoja na sisi binadamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu haijatoa uzito unaostahili kibajeti kwa eneo hili. Nichukue fursa hii kuiomba Wizara kufuatilia maombi yangu ya mara kwa mara ya kuja Jimboni kwangu kuona athari mbalimbali zinazosababishwa na mabadiliko ya tabianchi ukanda wa tambarare katika Kata za Arusha Chini, Mabogini, Old Moshi Magharibi na Kahe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri yetu imefanya jitihada na kupata mshirika toka Ujerumani Jiji la Kiel ambalo linatusaidia sana kufanikisha mradi wa mazingira wenye lengo la kurejesha miti ya asili ambayo ni rafiki wa mazingira katika eneo letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana Mheshimiwa Waziri aje aone jitihada hii, aitambue na Serikali ione jinsi ya kuchangia na kupanua mradi huu kuhusu manufaa ya maeneo mengine katika Taifa.