Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Januari Yusuph Makamba Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira kwa kazi kubwa anayoifanya pamoja na Naibu Waziri Mheshimiwa Mussa Sima bila kuwasahau wafanyakazi wa Wizara hiii kwa kusimamia na kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na umuhimu wa mazingira naishauri Serikali itenge fedha za ndani katika bajeti ili kuweza kutekeleza majukumu yake na sio kutenga fedha za wahisani kutoka nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri katika kampeni ya upandaji miti Serikali ione haja sasa ya kupanda miti yenye faida zaidi ya moja, nashauri ipandwe miti mingi ya matunda kwanza tutahifadhi mazingira pia yatapatikana matunda ambayo ni muhimu kwa binadamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mifuko ya plastiki si vizuri kwa mazingira na naunga mkono usitishwaji wake. Ushauri maelekezo ya awali ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ni kutumia Kiwanda cha Mgololo kutengeneza mifuko mbadala na kiwanda hicho hutumia malighafi ya misitu (miti).

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ihamasishe wananchi kila mkoa kuanza kulima kilimo cha miti ambayo itatumika katika viwanda vitakavyotengeneza mifuko hiyo kikiwemo Kiwanda cha Mgololo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya mita 60 ipitiwe upya maana kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi maeneo ikiwemo mito maziwa (Victoria) na kadhalika na kusababisha migongano isiyo ya lazima katika ya Serikali na wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna utupwaji hovyo wa chupa za maji, juice pembezoni mwa barabara kuu ziendazo mikoani. Serikali ifanye utaratibu wa kutoa elimu hususan kwa wafanyakazi wa magari ya abiria licha ya kuwa na vyombo ndani ya mabasi vya kuhifadhia taka, lakini bado utupwaji upo na unaharibu mazingira. Hivyo, wafanyakazi hao wa magari ya abiria wapewe elimu ya kutosha ya uhifadhi wa mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali na Wizara ya Nishati ili kupunguza ukatwaji wa miti ambayo hutumika kusambaza umeme mijini na vijijini na Wizara ya Nishati ianze mara moja utumiaji wa nguzo za zege ambazo kila mara imeahidi kutumia ili sasa kuepuka kukata miti mingi ambayo itapelekea nchi kugeuka jangwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naomba Mungu ampe Mheshimiwa Waziri umri mrefu na afya njema katika kuyatekeleza majukumu yako ya kila siku.