Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kupoteza muda, nianze kwa ni-declare interest kwamba mimi ni mmoja wa wanaohitaji Muungano na Wazanzibar wengi wanauhitaji, lakini niformula tu ya kuuendesha muungano huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, nichukue fursa hii kuwashukuru sana viongozi wetu wawili wakubwa; Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Mheshimiwa Rais Dkt. Ali Mohamed Shein kwa ushirikiano mkubwa wa kutatua tatizo la mazingira ya hali ya VAT ya umeme na tumefikia mahali muafaka; mwezi huu wa Aprili, aliwahi kuzungumza Mheshimiwa Najma hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, ndugu yangu Mheshimiwa January Makamba, pamoja na kuambiwa na Mawaziri wenzake ni Mzanzibar, akubali hivyo hivyo. Ameonesha uwezo mkubwa sana katika Mawaziri ambao wameitwa Zanzibar wakafika kwa wakati, mmojawapo ni yeye. Haya ndiyo malezi mazuri binadamu anatakiwa kulelewa. Ameonyesha ushirikiano kwa hali na mali bila kujali mvua wala jua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sitamfanyia haki Mheshimiwa Naibu Waziri wake tumemshuhudia sana katika kutatua matatizo hayo. Pia nitakuwa sijamfanyia haki ndugu yangu, jirani yangu Mheshimiwa Keissy. Nakushukuru sana kwa utulivu wake alioonesha kwa kipindi kirefu baada ya kero hizi za Muungano. Ametulia sana Mheshimiwa Keissy, namshukuru sana na huu ndiyo uungwana.

Mheshimiwa Mwenyekiti,…

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: …nataka kuuliza…

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: …nini Muungano?…

MHE. ALLY K. MOHAMED: Taarifa.

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: …maana ya formula ya Muungano?

MHE. ALLY K. MOHAMED: Nataka nimpe taarifa huyu.

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: …umuhimu wa kuungana ni watu kuwa pamoja, kushirikiana katika nyanja mbalimbali katika kuungana kiuchumi…

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: …ulinzi,…

MWENYEKITI: Taarifa

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: …maendeleo

MWENYEKITI: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampa taarifa mzungumzaji, anasema mimi nimetulia muda mrefu. Mimi sikuwa napinga Muungano, nilikuwa napinga habari ya bidhaa kutoka Zanzibar ambazo hazilipiwi ushuru, ndiyo nilikuwa napinga. Mambo mengine mimi…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Jaku, unapokea taarifa hiyo?

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba afute kauli yake. Kule Wazanzibar wanalipa ushuru, vinginevyo kwa vyovyote vile kungekuwa hakuna Serikali pale bila kulipa ushuru. Naomba umruhusu afute kauli yake kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Siyo kauli ya kiungwana aliyoitumia. Hiyo siyo kauli ya kiungwana, yeye atetee mambo yake kule Nkasi; maji hakuna, barabara ndiyo vya kutetea. Wazanzibar wapo wenyewe wasemaji.Wakuu wa Dunia walishirikiana katika Jumuiya za Afrika Mashariki waliomba European Union kwa mashirikiano makubwa sana, lakini jambo la kushangaza na la kusikitisha, nije katika bidhaa za biashara hasa kutoka upande wa Zanzibar kuja kutafuta soko hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni geti kubwa la Bandari ya Tanzania Bara na ndiyo soko kubwa lenye walaji wengi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kati. Hili suala limekuwa ni la muda mrefu, vinginevyo labda ifutwe hii kauli. Kuna mahali Kenya inataka kwenda, Rwanda inataka kwenda na Burundi inataka kwenda, lazima ipite katika gateway kubwa hii ya Bandari ya Dar es Salaam. Sasa patafutwe njia. Hili suala limekuwa la muda mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Zanzibar wapo katika Jukuiya ya Afrika Mashariki, vinginevyo, watumwe Wabunge wetu wa Afrika Mashariki na Kati wapeleke hoja binafsi Zanzibar itolewe katika hili. Hili ni soko lenye walaji karibu milioni mbili na kuendelea. Hili ni jambo la kufikiriwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kushangaza Mheshimiwa Waziri Dkt. Mpango lilitokea tatizo la Kenya, bidhaa za Kenya kuja huku ilikuwa maziwa sijui na cigarrete na bidhaa za hapa kwenda kule, tatizo likatatuliwa mara moja. Sisi ndugu wa damu. Mheshimiwa January utapa kazi kubwa sana haya mambo, lazima ufuatilie; na yote utakuwa masuuli hata kwa Mwenyezi Mungu. Haya ni mambo ya kuyafikiria. Mmetatua kero za mbali za karibu mmeziacha! Lah, hii siyo halali, mlifikirie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kupoteza muda, Mheshimiwa Dada yangu Mheshimiwa Saada aliyazungumza Mashirika ya Muungano. Kwanza naipongeza sana Benki Kuu. Katika Shirika linalotoa pesa wakati, BoT; 4.5 ile inapatikana kwake tofauti na Mashirika mengine. Mheshimiwa Naibu Waziri yupo, Waziri wako hayupo, hii 4.5 tulikuwanayo ya mkataba tu, ni ya muda. Zanzibar imekua, population imekua, IMF walitumia kutokana na kigezo cha watu lakini mlifikirie. Mheshimiwa January lifuatilie suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mapato ya NBC, Zanzibar imo. Kuna Benki ya NMB, Zanzibar imo; kuna Postal Bank, Zanzibar imo; kuna TTCL, Zanzibar imo; kuna TCRA, Zanzibar imo; kuna TCAA, Zanzibar imo; imepata nini? Haya ni matatizo. Zanzibar imepata lini? Haielekei.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ajira za mambo ya Muungano Mheshimiwa January; kuna Jeshi, kuna migration, kuna Polisi, kuna Mambo ya Nje. Mnapogawa hizi kazi mfikirie mtapeleka namna gani Zanzibar, zinahitajika, Ajira imekuwa issue. Muungano wetu keshokutwa Mungu akijaalia unatimiza miaka 55, twende vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa uchumi siyo suala la Muungano, ndiyo hoja yangu ilipo; Zanzibar ina haki yake ya kutumikia Wazanzibar wake na Tanzania Bara ina haki ya kutumikia.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)