Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza napenda niipongeze Serikali ya Awamu ya Tano kwa jinsi inavyofanya kazi. Naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mheshimiwa January Makamba, Naibu wake, Katibu Mkuu pamoja na watendaji wote wa Wizara hii kwa hotuba waliyotuletea leo hapa Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nitazungumzia kuhusu mazingira. Kuanzia 1995, Mkoa wa Kigoma ulipata na wimbi kubwa la wakimbizi lakini pamoja na Mikoa ya jirani ikiwemo Kagera na Rukwa. Kutokana na wimbi kubwa la wakimbizi kufika katika mikoa hiyo ni ukweli usiopingika yametokea madhara makubwa ya uharibifu wa mazingira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, walipoingia watu kutoka Burundi kwa mara ya kwanza katika Wilaya ya Kasulu walifikia katika Kambi moja ya Mtabila, wakati huo mazingira yaliharibika kwani miti mingi ilikatwa. Kwa hiyo, unaweza kuona ni jinsi gani mazingira yalivyoweza kuharibika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata waliporudishwa walienda tena kwenye Kambi moja ya Nyarugusu ambayo ni kubwa, ina wakimbizi wa kutoka DRC na Warundi. Kwa hiyo, ni jinsi gani unaweza kuona mazingira katika Mkoa wa Kigoma yalivyoharibika na kule Kibondo vilevile ipo Kambi ya Nduta lakini Kakonko iko Kambi ya Mtendeli. Kwa hiyo, naiomba Serikali kwa kushirikiana na Shirika la UNHCR kuangalia ni jinsi gani zinaletwa pesa kwa ajili ya kunusuru mazingira katika mikoa hiyo ambayo ilipokea wakimbizi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naiomba Serikali iweze kuipatia Ofisi ya Makamu wa Rais pesa za kutosha kwa ajili ya kuweza kufanya ziara katika mikoa hiyo lakini kuweza kupeleka pesa kwa ajili ya kukabiliana na tatizo hili la mazingira. Ukienda kuangalia jinsi misitu ilivyoteketea, kwa kweli ni kilio kikubwa sana na wakati mwingine uharibifu wa mazingira unaendelea siyo kwamba eti mazingira yanahifadhiwa, hapana. Bado tuna kila sababu ya kuhakikisha Wizara hiyo inapatiwa pesa ili kwenda kunusuru mikoa ile ambayo imeathirika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Muungano, naomba wanafunzi waendelee kufundishwa umuhimu wa Muungano kuanzia darasa la kwanza mpaka vyuo vikuu. Kwa sababu watoto wakianza kufundishwa wakiwa bado ni watoto wataendelea kuupenda tangu mwanzo mpaka watakapoendelea kuwa wakubwa na wataendelea kuulinda kwa nguvu zao zote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, naunga mkono hoja, ahsante. (Makofi)