Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote naomba nichukue fursa hii nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa siku ya leo. Nichukue fursa hii pia kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa na nzuri anayofanya yeye na Serikali yake. Vile vile naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri Kapteni Mkuchika na Naibu wake, Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa, Katibu Mkuu na timu yake nzima kwa kazi nzuri wanayofanya. Naomba kushauri baadhi ya masuala ili kuboresha huduma na hasa katika Utumishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni suala la OPRAS; ni muhimu sana jambo hili lisisitizwe ili uadilifu na uwajibikaji uwe wa hali ya juu. Pia naomba Wizara iboreshe Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, sekretarieti hii hufanya kazi nzuri na kubwa, ingetumika pia kwa ajili ya ajira kwa taasisi za watu binafsi iwe sehemu ya kuwa benki ya wanaotafuta ajira. Wote wanaohitaji ajira waweze kuweka rekodi zao pale na wenye kuhitaji watumishi basi wapate orodha kutoka Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nashauri suala la watumishi wanaokaimu kwa muda mrefu utoke mwongozo na pawe na kanuni juu ya nafasi ya kukaimu; Babati Vijijini tunao wakuu wa idara wanaokaimu zaidi ya saba. Pia Serikali iangalie suala la kukaimisha watumishi bila utaratibu na inaleta gharama kwa halmashauri zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni suala la huduma kwa mteja (customer charter); suala hili likumbushwe kila wakati na itangazwe kwa wananchi, kila idara, taasisi iweke wazi suala la huduma kwa mteja (customer charter). Nashauri pia Sekretarieti ya Maadili ya Umma pia iweze kuweka mfumo wa kielektroniki ili tuweze kujaza fomu hizo kwa njia ya kielektroniki na pia tukihitaji kupata taarifa zingine na kujaza taarifa muhimu tuweze kujaza kwa njia ya kielektroniki (update information). Nashauri pia kuwa na mfumo mpya wa urasimishaji wa uendelezaji wa biashara (One Stop Center) hii itasaidia kupunguza gharama urasimu na muda wa kupata huduma.