Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza Waheshimiwa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu na wafanyakazi wote kwa kazi kubwa wanazofanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya watumishi wa Urambo,nashukuru sana kwa vituo viwili vya afya. Ahsante sana, ni msaada mkubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya ya Urambo ina kata 18 na kwa sasa tumepata vituo viwili vya afya, kwa heshima tunaomba vituo viwili vya afya kwenye kata zenye wakazi wengi na ziko kwenye barabara kubwa katika eneo la Songambele na Vumilia. Pia, tunaomba walimu na wafanyakazi wa afya ili wakafanye kazi kwenye vituo hivi, tunatanguliza shukrani.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Urambo ni moja ya Wilaya inayonufaika na Mfuko wa Rais wa Kujitegemea. Wananchi wa Urambo wameufurahia sana huduma ya mikopo. Je, Serikali inawaambia nini waliokuwa wanaendelea kupata huduma za Mfuko huu ambapo ghafla wameambiwa umesitishwa?Wafanyaje kuhusu marejesho? Je, isingekuwa vizuri Serikali kuwapa nafasi wanufaika na wanafakazi kukamilisha mikopo kwa mfano isingeweza kutoa noticena kusema kuanzia mwaka wa fedha 2020/2021 hakutakuwa na Mfuko wa Rais? Je, Serikali haioni kuwa Mfuko imesitishwa ghafla sana? Tunaomba Mfuko huu upewe muda wa kutosha ilivyo sasa ambapo taarifa imetolewa ghafla sana na masuala ya fedha hajakaa vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Urambo wanashukuru sana huduma ya MKURABITA. Tunaomba MKURABITA iendeleze huduma zake za biashara na kurasimisha ardhi ili wananchi wanufaike kwa kupata hati. Aidha, tunaomba fedha ziongezewe ili MKURABITA ifanye kazi kwa ufanisi zaidi.