Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Ajali Rashid Akibar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. AJALI R. AKBAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami nichangie katika Wizara hizi ambazo ni nyeti ambayo ni TAMISEMI pamoja na utawala bora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kutoa mchango wangu, katika Wizara hizi nyeti, nami niungane na Wabunge wenzangu kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais jinsi anavyoweza kugawa maendeleo ya nchi hii bila kujali Wapinzani au ni Chama Tawala. Kwa kweli, namsifu sana Mheshimiwa Rais na ni kweli, tunaona juhudi zake jinsi anavyofanya kazi kwelikweli. Kwa hiyo, nachukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kuwapongeza hawa watendaji Mawaziri ambao wapo katika Wizara zote hizi kwa maana ya TAMISEMI, lakini pamoja na Utawala Bora. Kwa kweli, wanafanya kazi pamoja na wasaidizi wao; nawapongeza ndugu yangu Mheshimiwa Jafo na kaka yangu Mheshimiwa Mkuchika. Kwa hiyo, moto mdundo waendelee kufanya kazi kama ilivyokusudiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizo nichukue nafasi hii naomba kutoa mchango wangu kwenye Wizara hii ya TAMISEMI. Namwomba Mheshimiwa Jafo, kwa kuwa tulikuwa wote kwenye ziara, nami nitoe mchango kwenye upande wa barabara. Kwa kweli, Halmashauri ya Wilaya ya Newala ina barabara ambazo ni nyingi sana, lakini ndiyo ambayo inalima karibu nusu ya korosho za Newala. Ila kutokana na mtandao, magari makubwa ambayo yanapita katika barabara zile, nimwambie Mheshimiwa Waziri Jafo, kwa kweli, zile barabara ni mbovu nasi Wilaya ya Newala, TARURA haina gari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nachukua nafasi hii kumwomba Mheshimiwa Jafo tupate angalao gari moja kama walivyopata Halmashauri za wilaya nyingine. Maana yule bwana anashindwa kufanya kazi na kwa hiyo, tutashindwa kusomba korosho katika Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Kwa hiyo, nachukua nafasi hii kuomba kwamba, nasi tunahitaji gari moja kwa ajili ya TARURA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, zile fedha ambazo zinagawanywa za TARURA sisi tumepata shilingi bilioni 900. Kwa kweli hizi fedha ni ndogo sana, sijui ni kigezo gani ambacho kinatumika, lakini zile barabara zote zilizopo pale wilayani ni mbovu na magari ambayo yanatumika kusomba zile korosho ni mabovu. Kwa hiyo, vinginvyo zile barabara zikiwa mbovu tutashindwa kwenda mbele kiuchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Jafo tuangalie kwamba kama zile barabara zitashindwa au kuongeza zile fedha, basi aangalie uwezekano yale maeneo korofi ambapo kuna milima, kwamba korosho zikishapakiwa magari yanashindwa kupanda, basi afanye utaratibu wa kuangalia kwamba, basi anaweka japo kilometa moja moja au mbili mbili za lami. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Mlima Miyuyu kwenda Ndanda; ule mlima kwa kweli ni mlima mkubwa na tulishamwandikia Mheshimiwa Waziri kuangalia uwezekano wa kuweza kupata angalau kilometa mbili za lami kutoka Miyuyu hadi kufikia Ndanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, barabara ya Mpalu hadi Mnyambe, wale watu wanalima sana korosho, lakini kutoka pale Mpalu kuna mlima ambao ni mkali sana. Magari yakienda pale yanashindwa kusomba korosho, Kwa kweli, hatuwezi kujenga barabara yote, lakini ile kilometa moja ambayo magari makubwa yanakwama tunaomba Mheshimiwa Jafo na Mheshimiwa Kandege Ndugu yangu waangalie uwezekano wa kuweka pale japo kilometa moja ya lami. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, pale inapoanzia chanzo cha maji Mitema pale Kitangali ambapo inakwenda barabara hadi kufika Mto Ngwele, ule mlima ni mkali sana, tunaomba vilevile japo kilometa ya lami. Ikumbukwe kwamba uchumi wote wa korosho unaotoka Newala kwa kiasi kikubwa unatoka Kitangali. Kwa hiyo, tungeomba kwamba kilometa nne au tano, itaufanya uchumi huu ukue sana na wa kitaifa maana yake tutakuwa tunapata mapato makubwa sana ya kitaifa. Mheshimiwa Kandege na Mheshimiwa Waziri Jafo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, nashukuru kwamba tumepata milioni 200 kwa ajili ya Kituo cha Afya Mkwedu. Kuna kituo cha afya kipo Chihangu, kile Kituo cha Afya Chihangu ni cha muda mrefu sana, kipo tangu mwaka 1969 na operesheni ndogo ndogo zinakwenda pale, lakini kwa kweli hatuna jengo la mama na mtoto. Kwa hiyo, niwaombe sana Mheshimiwa Jafo na Mheshimiwa Kandege wapeleke wataalam wakaangalie Kituo cha Afya Chihangu kwa sababu wale akinamama wanajifungulia jikoni na kulala wanalala nje, kwa hiyo inakuwa ni ngumu sana wakati wa mvua wale akinamama kuwa na sehemu ya kujistiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile zile nyumba za watumishi zote karibu zime-collapse tangu mwaka 1969 ambapo kituo cha afya kile kilikuwa kimejengwa mpaka leo kile kituo ni kibovu sana. Kama hiyo haitoshi, kile kituo cha afya kipo wazi kabisa, hakina fensi, maana yake hata kama wale watu ambao wanafanya utunzaji wa vile vifaa/rasilimali kwa mfano ile OPD ambayo ilikuwa imejengwa na Wajapan leo ulinzi wake unakuwa ni mgumu. Kwa hiyo, niwaombe sanawaende wakakague ili tuweze kufanya matengenezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili; niungane na Waheshimiwa Madiwani wenzangu; kwa mfano Halmashauri ya Wilaya ya Newala Vijijini ile ni kama Halmashauri mpya, haina mapato mengine. Baada ya kuwa hizi korosho zimeingia kwenye mtandao maana yake haina mapato, wale Madiwani wanakopwa mpaka vikao maana yake sasa hivi mpaka sasa wanadai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwombe sana Mheshimiwa Jafo tuangalie namna gani, kama ambavyo tumezungumza kwenye ziara ya Rais, namna gani hizi Halmashauri za Wilaya ambazo zinategemea kilimo hasa korosho na ushuru tulikuwa hatujapata, tutafanyaje ili kuwanusuru Madiwani hawa ambao wanadai malipo yao. Kwa hiyo, tuangalie namna nzuri ambayo tunaweza tukawasaidia kwa kuwalipa posho hawa Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, tuweze kuwasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Halmashauri ya Wilaya ya Newala ni pana sana kwa maana kwamba ina Kata karibu 22 ambayo ina mtawanyiko wa wakulima wa korosho. Je, ni namna gani tutawasaidia japo pikipiki kama itakuwa imeshindikana kuwapa mikopo ya magari, basi tuweze kuwanunulia japo pikipiki kama Waheshimiwa Wabunge wenzangu walivyotoa mchango kwamba tuangalie uwezekano wa hawa Waheshimiwa Madiwani ni namna gani tunaweza tukawawezesha kwa sababu wanatusaidia sana wakati wa kusimamia uchaguzi kwa maana ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Hawa Madiwani wanasafiri zaidi ya siku mbili kutoka Vijijini hadi kufika ilipo Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwombe sana Mheshimiwa Kandege na Mheshimiwa Waziri waangalie namna nzuri ambazo tunaweza tukawawezesha Waheshimiwa Madiwani hawa na waangalie vilevile ni namna gani wanaweza wakawalipa posho kwa vile vikao ambavyo wameweza kuwakopa kwa muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)