Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kupata fursa hii kuchangia katika hotuba ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI halikadhalika Utumishi na Utawala Bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaanza kwa mara nyingine kutoa pole kwa viongozi wangu wa chama hususan Kamanda wa anga, tunamwita Kamanda Mheshimiwa Freeman Aikaeli Mbowe na dada yetu mpendwa Mheshimiwa Esther Matiko kwa kukaa gerezani kwa dhuluma. Huu ni ushahidi mwingine wa uwepo wa hila. Ni ushahidi mwingine wa kutokuwepo au kwa upungufu ya Utawala Bora, watu wanakaa ndani kwa zaidi ya siku 104 kwa sababu ambazo zilionekana ni nyepesi na Mahakama Kuu ilitoa maamuzi inasema Mahakama ya Hakimu Mkazi ilikiuka kanuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ndiyo tunaanza kuangalia ni kwa kiwango gani katika nchi yetu tunasimamia Utawala Bora? Naendelea kumwambia Mheshimiwa Mbowe tunampenda sana, atabaki kuwa juu, juu, yuko mawinguni. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, kuna mwanazuoni mmoja anaitwa Twain Mark, aliwahi kusema kwamba uzalendo ni kui-support nchi yako, uzalendo ni kuipigania nchi yako kwa kila hali, uzalendo ni kuhakikisha muda wote unaangalia maslahi ya nchi yako na ikiwezekana au ikikuridhisha unaweza kui-support hata Serikali yako.

Mheshimiwa Mwenyekiti, anamaanisha nini? Kwa lugha ya kizungu alisema patriotism is supporting your country all the time and your government if it deserve it. Anasema ui- support nchi yako wakati wote, ui-support nchi yako kwa gharama na damu yoyote, lakini siyo lazima ui-support nchi yako kama hai- deserve hiyo aina ya support inayohitaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema haya? Kumekuwepo na malalamiko mengi ya mambo yanavyoenda ndivyo sivyo yanayofanywa na Serikali. Kumekuwepo na malalamiko mengi hasa kutoka kwa Vyama vya Upinzani, kuonekana tunatendewa ndivyo sivyo. Nikiongea haya, kuna watu hawawezi kunielewa kwa sababu wako tayari kui-support Serikali yao kwa jasho na damu na siyo nchi yao, kwa sababu wanaangalia kipi wanapata kutoka kwenye Serikali na siyo kwenye nchi husika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, TWAWEZA walifanya utafiti na moja kati ya matokeo waliyoyapata wakasema, raia wa Tanzania wanasema hawako huru kukosoa kauli za watawala. Kwamba raia wa Tanzania wanaogopa kusema ukweli kuhusu nchi yao inavyoendeshwa hiyo ni hatari sana kwa mustakabali mzima wa uendeshaji bora wa nchi yetu.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Utawala Bora, kumekuwepo na marufuku mbalimbali, wamesema wenzangu na hasa kuzuia kazi na shughuli za Vyama vya Siasa. Nataka kujua, Mheshimiwa Rais kama anafuata Katiba na Sheria, kama anafuata utawala bora alipata wapi mamlaka ya kuzuia kazi za kisiasa ambazo zipo kwa mujibu wa sheria ya nchi yetu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua Mheshimiwa Rais alipata wapi mamlaka; alipata wapi moral stand ya kutamka hadharani na kusema watoto wa kike wakipata ujauzito wasiendelee na shule, wakati ni haki yao ya msingi ya kwenda shule regardless ya mambo mengine tunayoyasema. Uthubutu wa kutaja maneno ambayo yanakiuka hata Katiba yenyewe aliyoapa kuilinda anaupata wapi? Hiyo ni swali langu la pili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu, tumekuwa tunalalamika vyombo vya dola kushiriki mambo yanayoonekana ni ya kisiasa, kuonekana vimeegemea kwenye mlango fulani wa chama. Tuliona kwenye vyombo vya habari, mmoja kati ya Polisi Tarime huko akitaja hadharani kidumu Chama cha Mapinduzi na wenzake wakaitikia na hakuchukuliwa hatua zozote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, tumeona kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano Ibara ya 74(14) kinachozuia Watendaji wa Tume kuwa wanachama wa Vyama vya Siasa, tumeona wiki iliyopita, somebody Mhagama Katibu wa Mkoa wa CCM anateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri. Hiyo tunaongelea utawala bora upi katika nchi yetu? Tunathamini utawala bora upi? Tunataka tuwasifu Serikali ya Awamu ya Tano kwa lipi? Kwa nini tuwe ma-patriot wa Serikali kama mnafanya mambo ambayo tunayaona yanaenda kinyume na utawala bora tunaousemea? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, tumeona impurity ya vyombo vya dola, impurity ya Polisi. Akwilina alipigwa risasi katika mkutano wa hadhara, yeye akipita kwenye daladala. Tuambiwe leo, uchunguzi umefikia wapi? Tukaambiwa faili limefungwa, huyo Askari specific aliyehusika, alichukuliwa hatua gani? Hiyo ni lazima mtuambie kama tuna-deal na suala linaloitwa utawala bora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, kumekuwapo na tuhuma ya vyombo vya dola kuteka, kutesa na wakati mwingine kuua raia wema. Wananchi wamekuwa wakilalamika, watu wamekuwa wakipotea na hatusikii kauli yoyote kutoka Serikalini na hata Wizara inayohusika. Sasa nataka tujue ukweli: Je, ni kweli hao Usalama wa Taifa wanahusika na hayo matendo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hayo yanatupa maswali kwa kile kilichomkuta Mohamed Dewji. Alitekwa katika filamu ambayo inaonekana haikuchezwa vizuri. Anatekwa katika mazingira yenye CCTV camera, anapelekwa kusikojulikana na anapatikana katika mazingira ambayo hayaeleweki. Hiyo inatupa shaka; je, tuko salama kiwango gani? Kama kweli vyombo vya dola vilifanya au havijafanya, mbona ule mchezo ulifanya wepesi na hatupewi majibu? Kwa nini majibu hayapatikani katika suala zima la kutekwa kwa Mohamed? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, nini kilitokea kwa Zacharia? Maana yake ilisemekana amekamata watu, amewapiga risasi, lakini inakuja kujulikana ni vyombo vya dola. Mnatushawishi kuamini hilo kwamba tunaowaamini tumewapa madaraka, wanayatumia vibaya. Kama ndivyo ilivyo, tunaiweka hii Serikali au tunaiweka nchi yetu katika mazingira yanayotia shaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaingia kwenye suala zima la uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Natambua mwaka huu tunaenda kuingia kwenye chaguzi za Serikali za Mitaa. Haijabishwa kokote kwamba Mheshimiwa Rais alitoa kauli kwamba Wakurugenzi watakaowatangaza Wapinzani kushinda uchaguzi kama wataendelea kulipwa mishahara au kupanda magari ya Umma. Haijapingwa kokote baada ya kusikia. Kama ndivyo ilivyo, haijapingwa kokote, tunaamini inabaki imesimama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami natoa wito, Mkurugenzi anayedhani anaweza kupora haki ya mamilioni ya Watanzania watakaokaa kwenye foleni na kupiga kura, mimi namwambia ahakikishe ukoo wake, ndugu zake, jamaa zake hawapo katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni gharama kubwa. Demokrasia ina maumivu makali sana. Watu wanaweka matumaini yao makubwa katika mifumo ya kubadilisha uongozi. Kama kuna mtu mmoja mjinga anaweza kuamua kupora haki kwa maslahi ya tumbo, ninakuhakikishia hapatatosha mwaka huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hilo halitoshi, tumeambiwa kanuni ziko wazi na ninasema kanuni ni lazima ziwe rafiki. Kanuni zisiwepo kwa lengo la kulinda chama kimoja, tumezisoma kanuni na tunaona zinatoa mwanya wa watu wetu kurubuniwa na kununuliwa, zinatoa mwanya wa kubambikiziwa kesi na kama ndivyo ilivyo, mtaelewa nini maana ya nguvu ya Umma. Demokrasia ikishindwa kufanya kazi, mjue kwamba watu watatafuta namna nyingine ya kujitetea na kujilinda. Nawatahadharisha sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaenda kwenye suala lingine dogo kabisa wakati namalizia. Naomba tuambiwe, hivyo vitambulisho vya ujasiliamali vilitoka katika mchakato upi? Ni makampuni gani yalishirikishwa na akina nani walipata tenda? Kwa sababu inaonekana kuna kitu kipo nyuma ya pazia hakijulikani. Sisi kama Wabunge watunga sera, hatujui mchakato uliohusika katika kupata Mkandarasi, hivyo vitambulisho vinaendaje? Mpaka sasa kimekusanywa kiasi gani cha fedha kwa vitambulisho vilivyogawiwa? (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)