Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Awali ya yote, nitumie nafasi hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu. La pili nitumie kwa dhati kabisa kumshukuru na kumpongeza Waziri wa TAMISEMI na Naibu wake kwa kazi ambazo wamekuwa wakifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda mimi nianzie alipoishia Mheshimiwa Mabula. Nadhani umewadia wakati kama Bunge na kama nchi tutazame mfumo wetu wa bajeti na budget process kwa sababu kwa uzoefu huu mdogo nilionao ambao tumekaa humu ndani, kila mwaka tunakuja tunalaumu kutokufikia malengo. Nadhani umewadia wakati wa ku-reflect na kuangalia, je, mfumo wetu wa kujadili na kupanga bajeti kama nchi unatatua matatizo tunayoyataka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, umefika wakati wa kukaa muda mwingi kuangalia revenue side kuliko expenditure side yaani tutumie muda mwingi kuangalia ni namna gani Serikali itapata mapato ili yaweze kwenda kutatua changamoto ambazo zinatukabili. Tusipofanya namna hii tutakuja kila siku hapa kuinyooshea kidole Serikali. Sisi wenyewe ndiyo tunapitisha hiyo bajeti ambayo kila mwaka tunaiona kwamba haifikii malengo lakini hatu-provide solution katika matatizo ambayo tunakabiliana nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nadhani umewadia wakati wa kuisaidia Serikali sisi kama Bunge na tuangalie kanuni zetu na sheria, je, mfumo wetu wa kujadili bajeti unajibu mahitaji yetu? Hili ni jambo la kwanza ambalo nilitaka niseme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nataka niongelee kidogo kuhusu TAMISEMI. Responsibility zilizoko katika Wizara ya TAMISEMI ni kubwa sana. Mahitaji yaliyoko TAMISEMI ni makubwa sana. Mfano pale kwetu Nzega tumejenga Kituo cha Afya cha Zogoro, Serikali ilitupatia fedha kama 500 million shillings, tumejenga nyumba za watumishi tano, tumejenga instruction zilizoletwa theatre, OPD, wodi ya akina mama, theatre ya akina mama kujifungulia na nyumba za wafanyakazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto inayotukabili leo ni vifaatiba. Wakati tuna majengo yaliyokamilika, vifaa tba hatuna. Naiomba Serikali na Mheshimiwa Waziri alifika pale akaiona, Naibu waziri alifika akaiona washughulikie suala hili. Mimi niwapongeze sana kwa maamuzi ya kutumia force account katika kujenga miundombinu katika kata zetu za vijiji vyetu, imeleta matokeo mazuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka niombe, tufanye stock taking, majengo yaliyopo sasa hivi ambayo yameshajengwa na nguvu za wananchi na mchango wa Serikali yana upungufu kiasi gani ili yaweze kutumika. Nzega tumejenga zahanati katika vijiji 17 ambazo ni nguvu za wananchi na tumefika katika level ya kuezeka. Tumetumia fedha zetu za ndani 700 million shillings kwa ajili ya ku-support infrastructure hizi lakini bado hazijakamilika. Naiomba TAMISEMI i-deploy team katika kila Halmashauri iende ikafanye tathmini ya miundombinu iliyopo ambayo haijakamilika tuweze kuikamilisha halafu tuanze phase two. Tunajua kwamba hatuwezi kuwa tumemaliza changamoto zote lakini angalau tuwe tuna kazi ambazo zimekamilika asilimia 100. Hili ni muhimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine nataka niongelee suala la TARURA. Umewadiwa wakati Wizara ya Fedha na Wizara ya TAMISEMI kukaa chini kutafuta chanzo sahihi, kwa sababu tusipokuwa na chanzo sahihi ambacho kiko dedicated kwa sheria ambacho kinaelekea kusaidia TARURA bado TARURA itabaki inapata ratio ya asilimia 30 wakati ina mzigo wa asilimia 70 mpaka 80 ya matatizo ya miundombinu. TARURA anachokipata ni kile ambacho kinakuwa shared na TANROADS. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, umefika wakati wa ku-evaluate, TARURA inafanya kazi kubwa sana na ni muhimu upande wa Central Government wakaelewa, wakulima wako vijijini, wanapovuna mazao yao wanahitaji kuyatoa vijijini kuyaleta kwenye barabara za TANROADS kwenda sokoni. Kwa hiyo, kama kutakuwa hakuna miundombinu sahihi ya kutoa mazao vijijini, mazao haya yatabaki shambani, yatakosa soko na tathmini zipo, post-harvest loss ni kubwa sana katika nchi yetu na mengine ni kwa sababu tu ya miundombinu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi ningeshauri wataalam wakae, tutafute vyanzo vya mapato. Tunaona chanzo cha mapato cha Sh.50 cha maji kinavyosaidia suala la maji, ni reliable source inaenda moja kwa moja kwenye Mfuko wa Maji kutatua changamoto za maji. Umewadia wakati wa kutazama reliable source ya TARURA ambayo itakuwa kisheria na ring fenced, itakayoenda moja kwa moja kwenye Mfuko wa Barabara wa TARURA. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka niiombe Serikali, Mheshimiwa Waziri, Nzega tulitengeneza mradi na tukaamua kuanza kuutekeleza kwa fedha zetu za ndani kabla ya kupata support ya kutoka Central Government. Tumeamua kuanzisha a transport hub katika Mji wa Nzega na tumeleta maandishi Serikalini, tume- improve revenue ya stendi ya Mji wa Nzega na sasa hivi tumeanza kuitumia temporary.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshapeleka maandiko Wizara ya Fedha na wataalam wa Wizara ya Fedha wamekuja hadi Halmashauri ya Mji wa Nzega, wametembelea na wameangalia viability ya mradi, tunaomba hizi fedha. Tuko tayari kusaini makubaliano na Wizara ya Fedha ili turudishe hizi fedha ziwe revolving funds kwa sababu tuna uwezo. Mapato tutakayoyapata we can pay back kama loan kutoka sehemu nyingine na hii itatuondolea matatizo katika Halmashauri yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nazungumzia hili kwa nguvu? Ni kwa sababu I am not a believer wa kufukuzana na mama ntilie, bodaboda na watu wadogo wadogo kwa ajili ya kukusanya mapato katika Halmashauri. Sasa hivi Central Government inachukua mapato ya Local Government na mimi ningewashauri chukueni na service levy ije tu Central Government kwa sababu kuna confusion katika Local Government. Service Levy iko kwenye sheria kabisa, anayetakiwa kutathmini na kujua turnover ni TRA, ile figure inapelekwa Halmashauri, Halmashauri aka-compute 0.03% lakini mfanyabiashara akifika kwenye Halmashauri anakutana na kigingi. Watu wa Halmashauri wanamwambia hii tathmini hapana na sisi tuna makadirio yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kumeanzishwa mtindo wa clustering, it is against the law. Kama tunaona Local Government control mechanism ya service levy Mheshimiwa Jafo wakabizini TRA kwa sababu sasa hivi hela zote zinaenda Central Government, wakabizini tu ili tupeleke kwenye Revenue Authority kila kitu, hii ni opinion yangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka niombe Serikali, Halmashauri ya Mji wa Nzega tumejenga shule ya wasichana, imekamilika. Tuna changamoto moja, tunaomba uongee na Wizara ya Nishati watupelekee umeme, iko porini wananchi walitoa eneo na wewe unaifahamu na Serikali naishukuru kwa support iliyotupa. Tunaomba ili shule hii ya watoto wa kike ya boarding school ya Mwanzoli mtusaidie umeme ufika ili watoto wetu wa kike waweze kwenda kusoma pale. (Makofi)

Jambo lingine ambalo nataka niiombe Serikali, tumejenga maabara, sisi tumekamilisha tumefikisha juu, tunaomba support kutoka Central Government. Tuna maabara 18, tunaomba mtusaidie kumalizia nyumba za walimu 10 katika Mji wa Nzega ili tuweze kutatua changamoto zinazotukabili katika Local Government.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naunga mkono hoja, ahsanteni sana. (Makofi)