Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mimi nitachangia katika eneo moja tu la utawala bora. Kwanza nataka nianze na msemo usemao, “Mgema akisifiwa tembo hulitia maji”. Sitaki kuufafanua nitauacha hivyohivyo tu uning’inie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuanza kwa kusema kwamba kukosolewa ndiko kunakomjenga mtu. Wanaokusifu hawakusaidii sana, ukikosolewa ndipo unapoona makosa yako. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana wakati nafanya research ya nini nitasema hapa nikaona kwamba IMF imetoa taarifa kwamba uchumi wetu utakua kwa asilimia 4 tu mwaka huu na mwaka ujao utakua kwa asilimia 4.2, kinyume na ambavyo tumeambiwa na bajeti inavyosema kwamba utakua kwa zaidi ya asilimia 6. Humu ndani tunajisifu kwamba uchumi unakua, wa pili Afrika, wa tatu Afrika, wa kwanza Afrika Mashariki, hiyo haisaidii kitu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nianze kwa kusema kwamba katika upande wa utawala bora kuna vitu vingi vya kuiga lakini tukifika kuwaambia viongozi wetu kwamba tuige hili tunaambiwa Tanzania haiigi kila kitu. Nitakuja na mfano mdogo tu mmoja mmoja kutoka Ethiopia, ndani ya miaka miwili Ethiopia imetoka kwenye dictatorship into democracy and now deep into good governance. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano nitakaoutoa ni wa mwanariadha ambaye anaitwa Feyisa Lilesa ambaye alishinda medali ya silver kule Rio De Janeiro. Yule anatoka Kabila la Oromo ambao ni wengi lakini kule kwao hawana nafasi ya kiuongozi. Alipokuwa kule in protest akafanya alama hii (hapa Msemaji alionesha alama) kuonesha kwamba Waoromo hawana uhuru ndani ya nchi yao wenyewe. Matokeo yake akabakia kulekule Brazil kama mkimbizi kwa miaka miwili. Jana amerudi kwao na ameitwa na Waziri Mkuu ameambiwa njoo nyumbani hata kama uliikosoa nchi yako ukiwa nje, rudi nyumbani uje ujenge Taifa. On top of that akarudishiwa zawadi yake ya Olimpiki ambayo alikuwa apewe ya dola 17,000, look at that level. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi hapa Profesa Assad amekwenda nje na amesema maoni kuikosoa Serikali, tunasema uzalendo, hautakiwi ukosoe nje ya nchi. Utakosoaje ndani ya nchi wakati hakuna nafasi ya kukosoa? Utakosoaje ndani ya nchi wakati uhuru wa kujieleza na uhuru wa kujikusanya haupo kabisa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tukisema utawala bora tutizame na mengine. Utawala bora siyo maneno tu, utawala bora lazima uendane na haki, usawa, uadilifu na imani, lazima uendane na Katiba na sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza mifano ya kuonesha kwamba we still have a lot to do katika utawala bora. Nianze na uhuru wa kujikusanya, uhuru wa siasa. Kwa mujibu wa Katiba ya nchi hii na sheria, hakuna mwenye uwezo wa kusema kwamba nasimamisha siasa mpaka wakati wa uchaguzi, hakuna kisheria wala kikatiba. Kwa mujibu wa sheria hakuna mwenye uwezo wa kusema kwamba nasimamisha siasa mpaka wakati wa uchaguzi, hakuna kisheria na kikatiba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyama vipo kufanya siasa wakati wowote. Hata kauli ile itoke juu kiasi gani, ni kauli batili, haramu, mutlaq. Hata kama imetoka juu kiasi gani, huwezi kuwazuia wananchi wako wasifanye siasa eti kwa sababu wajenge nchi. Nchi ni pamoja na kufanya siasa na kukosoa ndiyo kujenga nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi vyama vingine vya siasa haviruhusiwi kufanya mikutano na Polisi mpaka sasa wanashindwa hoja. Hoja yao ni simple intelijensia. Intelijensia yenyewe haionyeshi kama ya kisayansi ya kisasa. Aah, maana yake Chama cha CUF kitazuia vyama vingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano uliotolewa, CUF watazuia ACT wasifanye mikutano. Hivi CUF ni chama cha fujo? Hivi huoni kwamba unakiweka pabaya Chama cha CUF kwamba ni chama cha fujo kinataka kuzuia mikutano ya vyama vingine? Au mnataka kukifuta na CUF vilevile! Kwa sababu kama chama kinafanya fujo kila siku za kuzuia mikutano ya vyama vingine nacho kifutwe? Siamini kama CUF wanafanya hivyo. Hawafanyi hivyo kwa sababu ni their interest vile vile na wao wakifanya mikutano yao wengine wasitumike kuwazuia. Hilo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni jambo ambalo sioni kama linaendana na utawala bora, nalo ni taasisi zetu za kiulinzi kupokea zawadi. Jana nimeona Polisi wanapokea vifaa gani sijui kutoka NMB. Mara utasikia wamejengewa vibanda, mara sijui vitu gani how can you do that? Mtu ambaye anakuzawaidia utawezaje kum-counter? Utawezaje kum-check akifanya makosa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Taasisi ya Polisi au Jeshi ama wengine wanawekewa vote; kwa nini waende wakajidhalilishe kwa kupekewa vibanda viwili, vitatu vya kujengwa barabarani? Huo siyo utawala bora, kwa sababu huyo ambaye amekuzawadia huwezi tena kumkagua. Kwa mujibu wa sheria yetu ya rushwa, anayepokea na anayetoa wote ni rushwa. Kwa hiyo, Polisi nao wanapokea rushwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni Miswada; tunakuja hapa ndani ya Bunge letu, Miswada mingi utaona hata haitoi fursa nyingine za kisheria. Unashangaa wanasheria wetu wanaoleta Miswada Bungeni wanayo dhana ya utawala bora ndani ya akili zao? Kama hawana, kwa nini basi muwaache walete Miswada kila siku. Ndani ya Kamati yetu ya Katiba na Sheria tunasema mbona hapa hakuna fursa ya rufaa? Mbona hapa hakuna kitu gani? Utawala bora bado haujaingia katika akili zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nataka kulisemea ni suala la TAKUKURU. Watu wanashitakiwa kwa very grievous offences kwa mfano utakatishaji fedha au uhujumu uchumi, lakini wanatangaziwa dunia nzima, wanahukumiwa kabla hawajafika mahakamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana nimeona kesi moja, mama mmoja anashitakiwa, anapelekwa mahakamani, TAKUKURU wanatoa Press Conference. Tayari umeshamhukumu mtu yule katika public. Kwa hiyo, huu siyo utawala bora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni muundo wa kuhoji watu hadharani. Umekuwa mtindo sana katika nchi yetu ya Tanzania kwamba Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa anaweza kuwaita watu akawahoji katika hadhara na hata mkuu wetu wa nchi anafanya. Kusema kweli taratibu za kumhoji mfanyakazi zipo; taratibu za kumkosoa mfanyakazi zipo, zimewekwa kisheria. Sasa kwa nini umwite hadharani, uende ukamuue kwa pressure na kitu gani, unamdhalilisha mbele za watu ajibu maswali papo kwa papo wakati ungeweza kuwa naye ofisini? Huu siyo utawala bora. Siyo utawala bora kabisa kwa sababu humtendei haki mfanyakazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mwingine, juzi nimeona, nafikiri Mkuu wa Mkoa wa Iringa, anamwambia mtu wa benki aende akafungue benki aje na nyaraka siku ambayo siyo ya kazi. Aende akafungue achukue nyaraka wakati ambao siyo wa kazi. Anamwambia wewe si ndio Meneja bwana, nenda kafungue lete nyaraka hapa. This is not utawala bora. Jamani, utawala bora deserves more than that. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kwangu mimi, utawala bora ni financial governance. Ripoti ya CAG inaonyesha kwamba utawala bora is far from dream to us. Madudu ambayo yanaendelea ndani ya Serikali katika upande wa fedha yanatisha. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)