Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi hii. Nami kabla sijazungumza maeneno mengi naomba niounge mkono hoja, lakini nimpongeze sana mtoa hoja Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na wasaidizi wake Mawaziri; Mheshimiwa Jenista Mhangama pamoja na Mheshimiwa Angella Kairuki na Manaibu Waziri kwenye Wizara hii kwa kazi kubwa waliyoifanya na kwa namna kwa kweli ambavyo wamewasilisha hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa umakini mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba kwenye sekta ya madini yapo maeneo ambayo yamezunguzwa kwa urefu kidogo na Waheshimiwa Wabunge na moja ya jambo ambalo limeongelewa hapa ni habari ya kudhibiti utoroshaji wa madini, kwamba Wizara ionge msukumo kwenye utoroshaji wa madini. Mheshimiwa Waziri Mkuu amekuwa champion mkubwa sana kwenye jambo hili, kama mtakumbuka aliitisha mkutano na Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa wote nchini kwa ajili ya uanzishwaji wa msoko ya madini nchini. Tulikaa kwa siku mbili nzima na yeye mwenyewe alitoa msimamo mkubwa na hata wakati kwa kwenda kuzindua soko la madini kule Geita, yeye Mwenyewe Mheshimiwa Waziri Mkuu alichukua kazi hiyo ya kuzindua soko. Pia akatoa maelekezo kwa Waheshimiwa Wakuu Mikoa wote kwamba ifikapo Juni 30 mwaka huu, kila Mkoa kuwa na masoko ya madini mbalimbali.

Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye ndiye mtoa hoja wetu leo kwa kweli amekuwa msimamizi mkubwa sana wa jambo hili. Hata hivyo, Wizara ya Madini tunafanya kazi ya kubwa ya kusimamia utoroshaji wa madini kama tulivyoeleza. Kwanza mambo yaliyokuwa yanasababisha utoroshaji wa madini ni kodi ambazo sio rafiki. Watu walikuwa wanaona nafuu kwenda kuuza kwenye masoko yasiyojulikana kwa sababu ya uwepo wa kodi nyingi ulikuwa unawafanya waogope kwenda kwenye masoko hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi hizo ambazo zilikuwa kero kama ambavyo wao walisema Serikali imechukua hatua kubwa kabisa ya kuziondoa; VAT withholding tax zimeondolewa ili kuwaruhusu sasa wachimbaji wetu waweze kufanya biashara katika mazingira rahisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunaongeza sasa Vituo vya Ukaguzi wa Madini. Sasa hivi tunavyo vituo 87 kote nchini, tunataka tuviongeze mpaka vifike 166 na kazi tunaanza kuifanya mapema ili tuweze kusimamia vizuri madini haya ambayo yanasafirisha nje ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kapufi ameelezea habari ya wachimbaji wadogo wanapongia mikataba na wageni kwenye uchimbaji. Nataka nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Kapufi na Waheshimiwa Wabunge na wachimbaji wote nchini, Serikali imewapa fursa Watanzania kutafua mbia au mtu wa kushirikiana naye kwenye kazi ya uchimbaji kutoka mahali popote. Wajibu ambao anao huyu anayetafuata mbia, kwanza lazima huo mkataba wanaoingia waulete Serikalini ili Serikali iweze kuagalia kama unakinzana na sheria zetu za ndani, lakini kuangalia kama Mtanzania huyu hatanyonywa. Tunayo mifano mahali pengi Watanzania wamengia mikataba na wageni, ukienda kuangalia mwenye leseni ni Mtanzania, lakini kila anachopata Mtanzania ni asilimia tano hadi kumi. Hatuwezi tukakubali Watanzania wakanyonywa na Serikali yao ipo kwa ajili ya kuangalia maslahi yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwatoe wasiwasi na niwaombe wale wote wanaopata wawekezaji toka nje, wawalete na mikataba yao ofisi kwetu kwenye Wizara ya Madini, mikataba ile iweze kusajiliwa ili ipate nguvu za kisheria kwa ajili ya kusimamiwa, sisi tutawapa kila aina ya support watakayoihitaji kutoka kwetu. Naomba vile vile niwatoe wasiwasi Watanzania kwamba kuna utaratibu wa watu wanaofanya kazi ya utafiti kutengeneza taarifa za kupika ili waweze kuziuza kwa bei kubwa kwa watu kutoka nje. Jambo hilo kama Wizara linatufedhehesha sana, lakini zaidi sana linatuondelea imani kwa wawekezaji kutoka nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeamua Wizara ya Madini, tunataka tuanzishe mchakato wa kuanzisha Bodi itakayowasajili Wajiolojia wote hapa nchini ili kila mmoja anapofanya kazi ya utafiti na kutoa geological report aweze kubanwa na sharia, asiweze kupika matokeo kwa ajili ya kutafuta fedha.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa…

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na ahsante sana.