Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naunga mkono hotuba ya Waziri Mkuu. Natoa shukrani kwa Serikali kwa ujenzi wa daraja la Mto Momba linalounganisha Mikoa miwili y Songwe na Rukwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na shukrani hizo, tunaomba sasa barabara ya kutoka Kilyamatundu hadi Kasansa, barabara inayounganisha Mikoa mitatu ya Rukwa, Songwe na Katavi. Barabara hiyo sasa itengewe fedha kwa ajili ya usanifu ili hatimaye ijengwe kwa kiwango cha lami kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutengewa pesa kwa ajili ya kumalizia maboma ya majengo ya madarasa na nyumba za walimu. Katika Jimbo la Kwela lililopo Sumbawanga DC upande wa elimu tunayo maboma 259. Zahanati tunayo maboma 32 ambayo yamejengwa na wananchi yanahitaji fedha za kumalizia. Vituo vya afya vilivyoanzishwa na wananchi saba (7) vinahitaji fedha ili vimaliziwe vianze kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tuna upungufu wa watumishi. Upande wa afya tuna upungufu wa watumishi 667 katika Halmashauri ya Sumbawanga DC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri Serikali itoe mgao wa miradi ya maendeleo na watumishi kwa uwiano ulio sawa bila kuwa na upendeleo. Baadhi ya Mawaziri wanapendelea maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Ntendo - Muze, tunaomba ijengwe kwa kiwango cha lami. Tunashukuru Serikali katika bajeti ya mwaka 2018/2019 ilitengewa fedha na kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami kilomita 2. Kutokana na umuhimu wa barabara hiyo, tunaomba kilomita ziongezeke walau ziwe kilomita 5 ili kuwatendea haki wananchi kwani barabara hii ina umuhimu mkubwa sana kwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kukosekana kwa gari katika Kituo cha Afya Milepa. Kituo hiki ni kwa muda mrefu Serikali iliahidi kukipatia gari lakini hadi leo hakijapatiwa. Matokeo yake kimekuwa kikipoteza akina mama wajawazito wengi baada ya kukosa gari la kuwasafirisha kuwapeleka katika hospitali za rufaa kwa ujuzi ulio juu zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Makamu wa Rais, Mheshimiwa Samia Hassan Suluhu, wakati wa Kampeni za Uchaguzi za mwaka 2015 alitoa ahadi ya kujenga barabara ya Mtowisa – Ng’ongo - Kristu Mfalme kwa kiwango cha changarawe. Tunaomba ahadi hiyo itekelezwe ili kumpa heshima mama yetu na kuondoa shida wanayopata wananchi wa eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maji bado ni tatizo kubwa katika nchi yetu hususan Jimbo langu la Kwela, nikianzia na Serikali kutucheleweshea kibali cha kutangaza mradi wa maji wa Vijiji kumi unaoitwa MUZE GROUP. Tunaomba kibali hicho kitolewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kushindwa kulipa fedha kwa wakandarasi mfano Mradi wa Maji Ikozi. Naomba Serikali iwalipe wakandarasi hawa ili wasaidie upatikanaji wa maji kwa wananchi wangu.