Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kuipongeza Serikali kwa juhudi kubwa sana za kuwaletea wananchi maendeleo. Nawapongeza viongozi wetu Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mheshimiwa Waziri Mkuu na Mawaziri wote wa Ofisi ya Waziri Mkuu/Bunge kwa utendaji wa kazi ulio bora katika kuongeza juhudi za kuwatumikia wananchi wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, masuala ya Muungano; naipongeza Serikali yangu kupitia kikao chake cha Baraza la Mawaziri kuridhia kuondosha kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwa kiwango cha asilimia sifuri kwa umeme unaouzwa kwa Shirika la Umeme la Zanzibar (ZECO) kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) sambamba na kufuta malimbikizo ya deni la VAT la shilingi bilioni 22.9 kwa Shirika la umeme (ZECO).

Mheshimiwa Spika, ulinzi na usalama; navipongeza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kazi kubwa wanayofanya kuhakikisha nchi yetu iko salama na ulinzi wa raia na mali zao.

Mheshimiwa Spika, miundombinu; Serikali imefanya juhudi kubwa katika kuimarisha sekta hii kama viwanja vya ndege, barabara, reli na hasa reli ya mwendokasi, naipongeza Serikali pia. Nashauri kuongeza uwekezaji katika eneo la bahari kwa meli za abiria, mizigo na uvuvi.

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali iendelee na juhudi za kuweka mazingira wezeshi zaidi kwa wawekezaji wa ndani na wa nje ya nchi ili sekta ya uwekezaji izidi kuimarika ili kuongeza pato la Taifa, kuinua uchumi na kuongeza ajira kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Nawatakia utekelezaji mwema wa majukumu ya kazi zenu.