Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nami nimshukuru Mwenyezi Mungu lakini kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kutoa mchango wangu katika Bunge hili, nichukue fursa hii kuwashukuru wananchi wangu wa Jimbo la Singida Mjini walionipa ridhaa hii na mimi niwaahidi utumishi uliotukuka.
Pia nichukue fursa hii kushukuru Chama changu cha Mapinduzi, lakini pia niishukuru Kamati yangu ya Viwanda na nimpongeze pia Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji wake mzuri ambapo mambo mengi ambayo na mimi niliyatarajia sasa nimeyaona yakiwa humo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende moja kwa moja kwenye kuchangia hoja ya viwanda. Nianze na EPZA kwa maana ya pale Kurasini, eneo lile ni muhimu sana na niipongeze sana Serikali kwa uwekezaji mkubwa ambao unaendelea pale. Mambo yaliyomo mule ni mengi sana na nimejifunza vitu vingi mle ndani na ni vizuri sana Watanzania wakajua kwamba leo hii Serikali yetu kwenda kwenye viwanda wala haijakosea. Kuna uwekezaji mkubwa na pale wanatengeneza jeans ya grade A, suruali ile inauzwa Marekani, Uingereza na German, ina-compete kwenye soko la Kimataifa. Hali kadhalika pale wanatengeneza mpaka ATM card mpaka voucher tunayoweza kuitumua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hoja yangu ni nini hapa? Hatuwezi kuendelea kuwa-entertain wawekezaji halafu wakawekeza na sisi tukabaki tu kutumika. Niiombe Serikali ifike mahali tuwe na mpango wa ku-adopt teknolojia kutoka kwa wenzetu hawa wageni lakini isitoshe ku-adopt kama inawezekana kuinunua teknolojia ifike mahali tuinunue teknolojia. Baada ya huo muda wakiweza kuondoka na sisi tuweze kuendesha hivyo viwanda ambavyo vipo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine ni la ajira. Tumezungumzia kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi asilimia 40% ya ajira. Nataka jambo hili tuliweke wazi. Tunao vijana zaidi ya 800,000 wanaingia mtaani kila mwaka na wote hawa tunazungumzia ajira. Hapa palihitaji ufafanuzi mpana kidogo. Najua utafiti ulifanyika ndani ya chama changu na Serikali yangu wanajua kabisa kwamba ajira hii inawezekana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tuliweke vizuri, ni vizuri tukaliweka katika mazingira ambayo yanaeleweka. Tunayo service industry, tuna kiwanda cha huduma, kote huku unakokuona hotelini, kwenye masoko, usafirishaji, mazingira haya yote yanazungumzia ajira ya Watanzania. Hoja yangu hapa ya msingi ni lazima sasa Serikali ijikite kwenda kuangalia mikataba ya hawa Watanzania wanaoajiriwa kwenye haya maeneo. Ni namna gani wanafaidika na namna gani wanaweza kujikimu kwenye maisha yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo wenzangu walizungumza awali lazima Serikali ijikite kwenye agro-product. Tuna kila sababu sasa ya kuwekeza zaidi kwa wakulima wetu ambao tunajua kila mkoa sasa hivi unazalisha na hiyo ago-product itatusaidia sasa kuboresha viwanda vyetu. Connectivity ionekane ya mkulima, ya mchuuzi na mtumiaji, hii pia inaongeza wigo wa ajira. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hoja ya kulinda viwanda vyetu vya ndani. Amejaribu kuizungumza Mheshimiwa Waziri namna ya kulinda viwanda vyetu vya ndani, mimi nilitaka nishauri na lazima tuliweke wazi. Ufafanuzi hapa ulitakiwa uwekwe bayana, tunapovipeleka viwanda vyetu vya ndani kwenye tenders kwa maana kwamba tumetangaza tender na vyenyewe vinakwenda ku-compete, kazi ile ni ngumu sana. Tunatakiwa katika asilimia 100% tuwape kwanza viwanda vya ndani asilimia 40% halafu asilimia 60% waingie kwenda ku-compete na viwanda vingine vya nje, hapa tutakuwa tumeweza kulinda viwanda vyetu vya ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe mfano mdogo, tuna Kiwanda cha TANALEC kinachotoa transformer bora East Africa na sisi Serikali mle ndani ni wabia. NDC wana 10% lakini TANESCO wana 20%, sisi ni wabia, maana yake sisi ni member wa Bodi ya TANALEC lakini kwa bahati mbaya sana tunaagiza transformer kutoka India. Ukiagiza transformer kutoka India, wenzetu Serikali ya India inatoa ruzuku ya 10% kwenye viwanda vyake vya ndani, kwa hiyo, uzalishaji unakuwa mkubwa inafikia mahali wanatafuta masoko kwa cheap price. Kwa hiyo, ukija ukiwaingiza TANELEC kwenda ku-compete wenzetu wanakuwa chini halafu hawa wa TANALEC wanakuwa wako juu na ukizingatia TANALEC wako Tanzania na sisi tunamiliki percent ya TANALEC. Kwa hiyo, niwaombe sana tunapokwenda kuhakikisha tunalinda viwanda vyetu vya ndani ni lazima tuzingatie mambo haya ya msingi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine, tuna kiwanda cha Urafiki, tuna asilimia 49% pale kwenye kiwanda kile na Wachina wana asilimia 51%, ndiyo wasemaji wakubwa wa kiwanda, lakini uzalishaji wa pale ni hafifu na Kamati imeeleza pale kuna madeni ya kutisha. Kwa hiyo, nimuombe sana Mheshimiwa Waziri tufike mahali kama ambavyo tumeshauri sisi ndiyo tu-hold share ya Kiwanda cha Urafiki. Sasa leo tunavaa khanga na vitenge kutoka China lakini tuna Kiwanda cha Urafiki, niombe sana Serikali iliangalie suala hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mahali siku za nyuma tulijaribu kulinda viwanda, niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge, tuna Mufindi Paper Mills. Kiwanda hiki cha Mufindi kinatumia rasilimali za Tanzania na ikumbukwe miaka ya nyuma 2007 cubic meter moja walikuwa wanauziwa nusu ya bei badala ya 28,000 wanauziwa 14,000 na bado ile pulp wanaisafirisha kwenda Kenya na wakitoka Kenya importation ya huku tumewapunguzia mpaka 10% Serikali inaingia hasara. Wakenya hawana misitu, misitu iko Tanzania. Kwa hiyo, niiombe Serikali iende ikaliangalie hili, hili jambo ni muhimu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niende moja kwa moja nizungumzie sekta ya ngozi. Mheshimiwa Waziri amezungumzia sekta ya ngozi hapa kwamba wataiangalia na wataboresha mpaka kufikia kiwango cha wet blue. Wet blue jamani ni sawa na kutengeneza raw material, ni sawa na kutengeneza ghafi. Leo hivi viwanda vilivyopo vya wet blue tunazungumzia temporary turning maana yake ni sawa na mtu anakwenda kwenye harusi unamuogesha tu halafu anaenda hana viatu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi leo tumepeleka fedha kwenye SIDO nimeona pale, zaidi ya shilingi bilioni sita lakini tunasafirisha ngozi hatuwezi kwenda huko. Mheshimiwa Waziri ni shahidi maghala yamejaa ngozi. Niombe sana Serikali sasa ichukue hatua ya haraka kuhusu suala hili. Vile viwanda ni temporary, umezungumzia viwanda nane hakuna viwanda nane Mheshimiwa Waziri, kama vinazidi sana ni vinne na bado ni temporary kwa hiyo Tanzania bado hatuna viwanda hivyo. Niombe sana jambo hili liangaliwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nishukuru tumezungumzia habari ya regulatory bodies, tu-harmonise vifanye kazi kwa pamoja kuondoa mlolongo mrefu ambao hauna tija. Jambo lingine tumezungumzia model, nimeona kwenye kitabu hapa, wenzetu wa Vietnam, China, Korea Kusini na wengine wote walianzia hapa tulipo. Kwa hiyo, niombe sana tuangalie hili tabaka la kati kwa maana ya middle class ndiko mahali ambapo tunatakiwa kujikita zaidi kuhakikisha kwamba Watanzania wanaweza kujikimu na maisha yao juu ya uwepo wa viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tunapozungumzia SIDO lazima tuweke connection na VETA. Hivi vitu lazima vihusiane, SIDO na VETA. Hatuwezi kuishia tu SIDO, VETA inafanya nini ili iweze kutusaidia? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Waziri jambo la mwisho kwamba sasa wakati umefika kama tumeamua Tanzania iwe nchi ya viwanda, tuwe na siku ya viwanda Tanzania. Jambo hili litawarahisishia wafanyabiashara na wenye viwanda kukutana na kujadili changamoto wanazokutana nazo hata kila mwaka, hata kila baada ya miezi sita, jambo hili litatusaidia sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niende mbali zaidi. Leo wenzetu wa Rwanda wanazalisha alizeti. Singida sisi ni maarufu sana kwa alizeti na bahati mbaya sana sijaona kama tunaenda kuanzisha kiwanda cha alizeti Singida, niombe sana suala hili liangaliwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia sisi Singida ni wafanyabiashara wazuri sana wa vitunguu. Mheshimiwa Waziri karibu sana tuje tuanzishe soko la Kimataifa pale Singida ili tuweze kuwasaidia wananchi wa pale. Rwanda leo wameweka 25% ya kodi hata Kenya wenyewe nao wanaweka lakini sisi tukitaka kuweka hapa mpaka tukaulize East Africa. Mheshimiwa Waziri naomba agenda hii uilete vizuri ili tuweze…
MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.