Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DKT. HAJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa ujumla katika utekelezaji wa majukumu yake katika kipindi hiki cha miaka mitatu yanaridhisha sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu unajikita katika kifungu 8.7, ukurasa 41 wa kitabu cha hotuba ya Waziri Mkuu, kuhusu huduma za uchumi; suala la migogoro ya ardhi kati ya wananchi na hifadhi/mapori tengefu. Katika Wilaya ya Malinyi/Morogoro wakazi wa vijiji karibu 18 vinavyopakana na Pori Tengefu la Kilombero wana mgogoro mkubwa wa marekebisho ya mipaka bado sio rafiki kwa wananchi. Sehemu kubwa ya mashamba yao yanayotumika kwa kilimo/ ufugaji yamechukuliwa na buffer zone ya Pori Tengefu la Kilombero.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hawa ni waathirika wa mabadiliko ya Sheria ya Wanyamapori ya 2009 ambapo sasa mashamba yao hayo ambayo walikuwa wakiyatumia hapo kabla ya 2009 yamenyang’amywa hivyo kusababisha kuwa na uhaba wa mashamba kwa shughuli zao za kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali warejee tena upya zoezi la kurekebisha mipaka ya Pori Tengefu la Kilombero ili kupunguza upana wa buffer zone kwa kuyaachia mashamba hayo yarudishwe kaika ardhi ya vijiji kwa faida ya maendeleo na ustawi ya wakazi wa Wilaya ya Malinyi, karibu watu 92,000 wameathirika na mgogoro huu wa mipaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.