Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mtemi Chenge nakushukuru kwa kunipa hizo dakika tano niweze kusema machache, japo nilikuwa na mlolongo mrefu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza mwaka jana nilipiga kelele juu ya Maziri kutofika Jimboni Ulyankulu, lakini leo napenda kuwashukuru Mawaziri karibu watano, sita, wamefika Jimboni Ulyankulu nawashukuru sana wamekuja kunitutia moyo kwa kazi zetu hizi za maendeleo, lakini nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa usimamizi wa shughuli za Serikali lakini kubwa zaidi ni lile la kuwa karibu sana na timu yetu ya Taifa. Kupitia yeye na Serikali niipongeze TTF ambayo nami ni sehemu yake. Tutaendelea kujipanga kuhakikisha timu yetu inafanya vizuri na niwaalike Waheshimiwa Wabunge mwezi Juni twende Misri kwenda kushangilia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo kwa haraka haraka ni suala la umeme, ile spidi ya umeme vijiji inaelekea imepungua kabisa. Sasa niwaombe wenzetu wa Nishati wajaribu kuihuisha tena, kazi hizi za umeme zinaleta maendeleo makubwa sana kwenye vijiji vyetu, basi haraka uwepo na utekelezaji maana yake yawezekana Mawaziri wakasema, wakiondoka huku nyuma watendaji wakawa si watu wazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mradi mzuri wa uchimbaji bwawa pale kwenye Kijiji ya Ichemba, niombe sana Wizara inayohusika kumekuwepo na upembuzi, lakini toka wameondoka hatujui kinachoendea

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni la barabara, kwa nafasi hii nimshukuru Mheshimiwa Kwandikwa, jirani yangu huyu, anapita kila wakati kuzikagua hizi barabara, Jimbo la Ulyankulu lina barabara kama tatu. Barabara ya Tabora Mjini kuja Ulyankulu; halafu barabara ya kutoka Kahama kwenda Ulyankulu mpaka Kaliua. Barabara hizi zinatusaidia kwa matatizo mbalimbali, jiografia ya jimbo la Ulyankulu si rafiki, nitatoa mfano, Kaliua tunajenga Hospitali ya Wilaya, tunajenga ofisi mbalimbali lakini wananchi wa jimbo la Ulyankulu hawapati huduma kule, wanapata Kahama pamoja na Tabora Mjini. Kwa hiyo, tunaposema maeneo ya utawala, najua hilo tumeshamwelewa Mheshimwa Rais, lakini najua mbele ya safari litakuja kukubalika tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la uchaguzi kwenye kata tatu bado nitaendelea kulisemea. Inakuwaje hawa watu wametupigia kura na Mheshimiwa Rais, lakini Serilkali imewazuia kupiga kura kwa ajili ya Madiwani, jambo hili sidhani kama lina majibu yaliyonyooka na Serikali inapindisha pindisha. Hebu Serikali ije na ufumbuzi wa haraka sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Waziri wa Afya pamoja na TAMISEMI kwa kutupatia shilingi milioni mia nne, tumeweza kutengeneza kituo vizuri cha pale Ulyankulu. Lakini imetuhamasisha na sisi kama wananchi kujenga vituo viwili vya afya vingine kwa nguvu zetu. Bahati nzuri Wilaya ya Kaliua ni Wilaya inayoongoza kwa mapato ya ndani kwenye Mkoa wetu wa Tabora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, tumeweza kujenga shule za sekondari na shule za msingi, sasa tuombe tu Serikali iharakishe hasa kwenye shule ya msingi vile vikwazo vikwazo vya ubora na nini, watusaidie kuvipunguza ili watoto waweze kuendelea na masomo vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nisingependa kuendelea na mambo mengi, nisingependa kengele inikute. Nakushukuru sana.