Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Rukia Ahmed Kassim

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. RUKIA AHMED KASSIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nami kuwezakupata nafasi hii ya kuchangia katika hotuba hii ya Waziri Mkuu. Naanza katika kitabu hiki cha Waziri Mkuu, ukurasa wa 11 unaozungumzia mfumko wa bei. Taarifa za kitabu hiki zinasema kwamba mfumko wa bei umepungua kwa wastan wa asilimia nne kwa mwaka 2018 hadi asilimia tatu kwa mwaka 2019. Jambo ambalo naliona liko tofauti kabisa, hali ya maisha ya mtanzania wa kawaida bado ni ngumu sana na kadri tunavyokwenda mbele maisha yanazidi kuwa magumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema haya kwa kutoa na mifano, mwaka 2018 Juni, Mtanzania wa kawaida alikuwa ananunua sukari kilo moja kwa Sh.2,100/=, leo Mtanzania huyu huyu ananunua sukari kwa Sh.2,400/=. Mwaka huo huo 2018, Mtanzania alikuwa ananunua maharage kilo moja Sh.1,700/=, mwaka huu 2019 ananunua kwa Sh.2,400/=. Mtanzania huyo huyo alikuwa ananunua tambi kilo moja Sh.1,700/=, lakini hivi sasa ananunua tambi Sh.2,500/= kwa kilo moja. Mafuta ya kula Mtanzania alikuwa ananunua lita moja ya mafuta Sh.1,100/=, lakini Mtanzania huyo huyo mwaka huu 2019 ananunua mafuta ya kula Sh.2,000/= kwa lita moja. Tulikuwa tunanunua mafuta ya petrol, kwa bei lita moja Sh.1,600/=, lakini hivi sasa ni Sh.2,206/=. Hapa napata ukakasi, naomba nipatiwe ufafanuzi. Je, mfumuko wa bei umepungua au umezidi? Mheshimiwa Waziri naomba awafafanulie Watanzania wajue, je, maisha yamezidi kuwa magumu au yamekuwa mazuri?

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hapo, nataka niende katika kitabu hikihiki cha Waziri Mkuu, ukurasa namba 44, unaozungumzia kupunguza kwa msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam. Ni kweli msongamano wa magari umepungua, tokea kujengwe lile daraja la juu la Mfugale. Pia tunategemea hali itazidi kuwa nzuri likimalizika kujengwa daraja la juu lile la makutano ya Ubungo, pamoja na daraja la Salender Bridge.Pia naishauri Serikali, Halmashauri ya Jiji sasa, ili na wao wajitahidi katika hili, waweze kutengeneza barabara zile za ndani, za mitaa, zilizoko Kariakoo wazitie lami, barabara za Kariakoo zile za mitaani, barabara za Ilala, za Magomeni ili sasa magari yaweze kupita kiurahisi katika zile barabara za mitaa kuliko kusubiri kupitia katika barabara zile kubwa tu,hapo nahisi kidogo foleni itaweza kupungua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo, naomba kutoa ushauri kwa Serikali. Wenzetu wa Senegal nchi yao ni ndogo tu, wana beaches nzuri, kama hizi zetu zilizopo Tanzania, Tanzania tumebahatika kuwa na beaches nzuri, tuna ufukwe wa bahari ambao ni wa kupendeza, una upepo wa kuvutia, lakini jiji hawajajitayarisha kuutengeneza huu mji wetu wakati huu mji wetu ni kioo cha Tanzania. Wageni wengi wanakuja hapa, hata sisi wenyewe, mji wetu ukijengwa, ukiwa katika mazingira mazuri na sisi pia tutafurahia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naishauri Serikali, Halmashari ya Jiji ya Dar es Salaam watengeneze fukwe zile za Oysterbay, badala ya kuziacha katika mazingira yale. Sasa hivi watengeneze public gym, ambayo watu wetu wataweza kwenda kufanya mazoezi, wataweza kupata afya bora, tutajenga vijana walio na afya bora na tutatengeneza Taifa ambalo lina vijana walio na afya bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia, watengeneze sehemu za kupumzikia, kama vile Zanzibar tulivyofanya Forodhani ili watoto wetu waweze kupata sehemu za kwenda kucheza, kupumzika, watu wazima waende pale kupumzika na kupunga upepo wa bahari na pia mji wetu utapendeza na utavutia hata kwa wageni watakaokuja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nitakwenda sasa kwenye barabara, kwanza naipongeza Serikali kwa kutekeleza Sera yake ya kuunganisha barabara za mikoa hizi kwa lami, wakiendelea na sera hii tutaweza kukuza uchumi, kitakuwa ni kichocheo cha kuleta maendeleo ya kiuchumi katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nawaomba watu wa barabara, yaani watu wa TANROADS, wajitahidi kutekeleza ile Sera na Sheria Namba 13 ya mwaka 2007 na Kanuni zake za mwaka 2019, waweze kuweka vigingi katika barabara, waweze kuangalia alama za barabarani, watoe taaluma kwa wananchi wetu, wasiharibu barabara. Kwa sababu watu wengi wanatoa alama za barabarani na hawajui adhabu yake ni nini. Wakiweza kutoa taaluma katika vyombo vya habari na watu wakajua kama unapotoa alama za barabarani kosa lake ni hili, watu wetu wataweza kuogopa na wataheshimu zile alama za barabarani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashauri watu wa TANROADS waweke watu maalumu ambao wataangalia alama zote za barabarani zitakazotolewa pamoja na rangi ambazo zinaweza kuwa zimefutika. Alama za barabarani zinasadia sana kuepusha ajali za mara kwa mara. Nasema hili kwa mfano, unapotoka Dar es Salam jioni ukafika huku Dodoma alfajiri, ukifika maeneo ya Gairo unakumbana na ukungu. Ukungu ule unakuwa huoni mbele yako kama kunakuja gari au haiji, huoni hata zile alama tena na barabara huioni, lakini zile alama za barabarani nyeupe zilizochorwa katikati ya barabara ndiyo alama pekee ambazo zinamwelekeza dereva wapi apite na wapi aelekee, bila alama zile nadhani magari mengi yangelianguka. Kwa hiyo, nashauri watu wa TANROAD wajitahidi, kila ambapo alama zile zimefutika wazirudishe na kila ambapo kuna alama za barabarani nyingine zilizotolewa wazirudishe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hapo, sasa nataka nijielekeze kwenye Jeshi la Zimamoto, mara kwa mara tunakumbana na maafa ya moto katika maeneo yetu, lakini Jeshi la Zimamoto halijajipanga kutoa taaluma kwa wananchi wetu. Kwa hiyo, naomba wawe na kitengo maalumu cha kutoa mafunzo, aidha kwenye Luninga, kwenye vyombo vya habari na watoe hata vingine kwa vitendo katika maeneo yetu. Kwa sababu ajali za moto, kuna mioto ya aina nne, kuna moto unaosababishwa na makaratasi au mbao. Moto huu unakuwa unazima kwa kupitia maji, watu wetu wakishajua pindi inapotokea moto wa namna hiiā€¦..

MWENYEKITI: Mheshimiwa Rukia ahsante sana.