Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Ahmed Ally Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Solwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. AHMED A. SALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika hoja hii. Kwanza kabisa, nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa hoja yake. Vilevile nimpongeze msaidizi wake mkuu, Dkt. Meru, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara alikuwa EPZ, ni Katibu Mkuu mmoja mzuri sana, anafanya kazi vizuri, tulikuwa naye, namfahamu atakusaidia sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ukitaka kuanzisha kiwanda au ili Tanzania iwe nchi ya viwanda, taasisi ya dunia inayotoa hali halisi ya mazingira mazuri ya kuanzisha viwanda nchi ya Tanzania ni ya 139 kati ya 184. Maana yake utaona Tanzania bado kuna vikwazo vingi sana katika kuanzisha bishara au viwanda katika nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri ameongea hoja nzuri sana lakini naomba nitoe mifano miwili, mitatu ili uone namna gani vikwazo hivi bado viko Tanzania. Ukienda TIC pale wako TRA, kipo Kitengo cha Ardhi na kipo Kitengo cha Uhamiaji lakini wale hawana mamlaka. Unapotuma application ya aina yoyote ili kupata huduma pale lazima sasa utoke tena uende Immigration au Ardhi. Wanasema kuna Benki ya Ardhi hawana, siyo kweli! Ukitaka kuwekeza pale wanaweza wakakupeleka kwenye pori ambalo linatakiwa lilipiwe, ufanye kazi kubwa, uanze kuendesha na mambo mengine mengi sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, TIC ni kitengo kizuri sana lakini Mheshimiwa Waziri ungefanya utafiti wa kina sana, One Stop Center siyo vile, ungeongeza na TBS na NEMC na wawe na maamuzi pale, ukipata certificate TIC wanakuambia nenda kafanye kazi, ukienda kuanzisha kiwanda, naomba ni-declare interest mimi nina kiwanda, raha ya ngoma uingie ucheze natengeneza air cleaner zipo hapa, mwaka mmoja na nusu kupata certificate ya TBS, mimi sijapata mpaka leo. Nimeenda kwa Katibu Mkuu na wewe nimekueleza mmenielewa. Sasa kama mimi nasumbuliwa hivi wengine inakuwaje? Kwa kweli TIC inatakiwa iwe ni One Stop Center. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, halafu umesema kuna viwanda zaidi ya 49,000, sawa, umefanya utafiti ni Watanzania wangapi wanamiliki na wageni wangapi wanamiliki? Tusipotazama huko tunakokwenda Watanzania watakuwa wasindikizaji na hauwezi kukataa wawekezaji wa nje kuja hakuna kitu kama hicho. Tunawahitaji kweli lakini kuwepo na mfumo mzuri. Mimi nitakuja na hoja binafsi namna gani bora ya kuwasaidia Watanzania waweze ku-penetrate kwenye suala zima la kumiliki viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme vikwazo vingine. Ukiwa na kiwanda cha maji TFDA anaingia humo, ukitaka kupata kibali TBS humo humo, OSHA humo humo na hao wote wanafanya kitu kimoja. Kwa nini wasikubaliane tu kwamba taasisi hii moja ikitoa kibali kwa ajili ya maji basi biashara yangu imeisha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda kwenye cement, ili uweze kuuza cement kwenye soko la Afrika Mashariki unatakiwa upate kibali cha Mkemia Mkuu ambapo unalipa 2.5% ya thamani lakini ukienda Kenya haipo, ukienda Uganda haipo. Unamwambia nini mwenye kiwanda? Ni kwamba ondoa kiwanda chako peleka Kenya, peleka Uganda ndiyo maana yake. Ndiyo maana sisi tumekuwa wa 139. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hapa wenye viwanda vya alizeti walisema wana uwezo wa kuwaajiri Watanzania milioni saba mpaka kumi lakini waondoe vikwazo vya kuagiza malighafi. Ukienda Uganda kupata kibali cha kuagiza malighafi ya mafuta ya alizeti kwa maana ya mbegu za alizeti ni miezi sita, Tanzania miaka saba, huu ni utafiti umefanyika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namuomba Mheshimiwa Waziri afanye utafiti wa kina sana, anaweza akaongea vizuri sana hapo lakini bado hatuko vizuri sana katika kuwasaidia Watanzania wawekeze. Kutana na wafanyabiashara wenye viwanda, wa kati na wa juu wakupe ya kwao uanzie pale, ukitoka na vile vitu vizuri ukavifanyie kazi kwa mfano suala zima la sera na kubadilisha sheria. Kwa mfano, mtu akiwekeza kiwanda cha mashudu hapa, akiagiza malighafi kwa ajili ya mashudu anapigwa ushuru mkubwa sana lakini ukileta mashudu kutoka Kenya unaingia bila VAT, ni msamaha tu! Maana yake unamwambia nini? Ondoa kiwanda chako cha mashudu peleka Kenya ili mashudu yaje Tanzania, ndio hivyo ilivyo. Kuna contradiction kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nina kiwanda cha air filter, naagiza malighafi kutoka nchi mbalimbali kama Korea na sehemu nyingine, unapigwa as if ni finished product lakini ukiagiza air filter ni 10% only finished product. Hivi una Mtanzania kweli unamsaidia? Yako mambo mengi tu lakini kwa kweli vikwazo ni vingi sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, bandari, Kenya wanatoa container milioni sita na nusu kwa mwaka lakini Tanzania ni container milioni moja na nusu wakati ule.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kuongelea transit containers siongelei container za ndani, hiyo ni biashara. Transit containers ni direct foreign income kwa nchi kama vile utalii tu, mtu ana-container lake anatoka DRC anakuja kulichukua hapa, anaacha pesa yake, anachukua container lake anaondoka.
MHE. AHMED A. SALUM: Tunapofanya maamuzi ndugu zangu, tuwe tunafanya utafiti nchi jirani kama Malawi, ninyi mnajua uhusiano wa Tanzania na Malawi.
MHE. AHMED A. SALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, Malawi ni nchi ambayo mahusiano yetu mnayajua wanatupiga vita kwenye bandari yetu hii, Kenya ni hivyo hivyo wanatupiga vita. Kwa hiyo, tunapofanya maamuzi ya aina yoyote ile tuwe tunatazama huku kwa sababu port ya Dar es Salam ni bandari. Sasa hivi ma-container yamepungua pale ni ma-container ya DRC, Zambia na Burundi yameondoka kwa sababu ya vikwazo vilivyokuwa ndani ya bandari yetu, yameondoka kabisa hivi hivi tu. Tumeweka VAT on the transit goods for what reason kuna checks point sita for what reason?
MHE. AHMED A. SALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja, dakika kumi ni ndogo sana, ahsante.