Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi kuchangia kwenye hotuba hii ya Waziri Mkuu. Nianze kwa kusema kwamba suala la kum-support na kumpa nguvu za kutosha Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano, Dkt. John Pombe Magufuli sio la majadiliano tena, ni suala la kumuunga mkono kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kila kitu. Na yale anayoyafanya hayawezi kutufaidisha sisi tuliopo, yatawafaidisha wanaokuja na huku mbele kama wenzetu wa upande wa pili wa Gaza kama watakuja kupata nafasi watafaidi haya matunda ambayo Rais anayafanya kwa sasa, kwenye miaka milioni 200 inayokuja huko mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze mambo matatu leo, la kwanza nataka nizungumze habari ya TANAPA. Shirika hili linatunza hifadhi 16 lakini hifadhi zenye faida ni tano tu, na juzi tumeongeza hifadhi nyingine za BBK, Burigi, Kimisi na hifadhi nyingine zimeongezeka nyingi, hifadhi tano ndiyo zenye faida. Na sasa shirika hili lina michango na kodi ambayo inalipwa kodi ndani ya kodi, likitoa mchango wa kujenga Kituo cha Afya Hunyari, Bunda kodi inakatwa, likilipa cooperative tax ndani ya kadi inakatwa, na tumezungumza sana na Kamati ya Bajeti nadhani imepewa hiyo taarifa. Ninafikiri Serikali ione namna gani ya kulipunguzia hili shirika hizi kodi ndani ya kodi ili liweze kujiendesha lenyewe kwa sababu lina mzigo mkubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, duniani kote mashirika kama haya huwa yanapewa ruzuku lakini TANAPA inajitegemea, kwa hiyo naomba waipe nafasi ili iweze kuleta namna ya kujenga miundombinu kwenye maeneo mbalimbali ili tuvutie wawekezaji na kuleta watalii wengi kama inavyoonesha kwenye hotuba ya Waziri Mkuu kwamba wameongezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nimeangalia kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri Mkuu, ukurasa wa 67 fursa za ajira, lakini nikasoma Mpango wa Maendeleo wa Taifa ukurasa wa 23 unasema; upatikanaji wa pembejeo, hatua iliyofikiwa ni kununuliwa kwa lita elfu mbili mia mbili sitini na tisa elfu na kilo elfu tatu vya viatilifu zenye thamani ya shilingi bilioni tisa na hivyo viatilifu vya bilioni tisa vinaua panya, nzige, wadudu viwavijeshi, sasa mimi leo nataka nizungumze fursa ya viwavijeshi na fursa ya vipepeo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika dunia ya leo kuna soko la mende, kuna soko la panya, kuna soko la mbwa, kuna soko la kwerea kwerea ambalo tunatumia bilioni tisa kuwaua, kuna soko la senene, kuna soko la kila kitu. Nchi yetu tumegawana katika maeneo mawili, eneo moja lina asilimia 36 ambayo ina mambo ya mapori haya, Mapori ya Akiba, TANAPA, maeneo tengefu na maeneo yote yaliyoko hapa. Eneo 64 ni letu sisi tunaotumia Watanzania, sasa kama tunalitumia tuna vitu vinaitwa mende, nyoka, mbwa, vinatakiwa kupata masoko ya nje, tutafute namna ya kufungua masoko hayo vinginevyo tunaua ajira, wamezungumza hapa ukurasa wa 67 fursa ya ajira tunatafuta fursa ya ajira katika mende.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mende leo ni zao kubwa sana Brazil, ukifuga mende wewe ni bilionea, kwa mfano mkate mmoja Brazili ni laki moja ambayo ni dola 44,000.4 ya Brazil ambayo ni sawasawa na laki moja na watu wanafuga mende sasa hivi wameanza kufuga Njombe. Leo tunapozungumza nyoka tunazungumza soko kubwa sana na viwanda vikubwa sana China. Kwa hiyo, tunafikiri kwamba kuanza leo watu wafuge nyoka kupeleka huko. Tunapozungumza kipepeo leo ni nafasi kubwa sana Malaysia na maeneo mengine.

Kwa hiyo tunapozungumza Kwelea kwelea, mmoja ni dola mia mbili hamsini ambayo ni pesa nyingi sana. Sisi tunasema tunatumia bilioni tisa kuua wadudu na kibaiologia na mimi ni mtu wa environment, unavyotumia ndege kuua wale wadudu maana yake unaua vyura vinavyohitajika, unaua nyoka wanaohitajika kule chini, unaua nzige wanaohitajika huko juu. Kwa hiyo, tunataka kujua ni namna gani eneo la uwekezaji litatumia viumbe hai hivi vilivyopo hapa kutengeneza njia kwa vijana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu wakenya wanashirika la KWS ambao wanatumia vibali hivi, kwa hiyo wenzetu wanatumia leo wanyama wetu hai, wanatumia mbwa, nyoka na membe kufunga katika maboksi kwenda nje. Kwa hiyo, tunaomba sasa Serikali najua Mheshimiwa Rais aliwahi kusema katika mambo, wakati huo tunafanya mambo ya ovyo, nasema yalikuwa mambo ya ovyo kupeleka twiga nje na wanyama wengine, lakini mzee alivyokuwa anakemea nchi sasa nchi imetulia, arudi aangalie ni fursa gani sasa ipo ambayo watu wanaweza kuitumia bila kuangalia mambo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kuzungumza hilo ili ieleweke kwamba kuna kuna soko kubwa sana la Afrika la wanyama hao. Pia kuna kitu kinaitwa konokono, Ghana ni chakula kibwa sana konokono na konokono kama mnavyomjua tunaita ni double entry anajizalisha mwenyewe, female and male yaani ukimfuga konokono mmoja akila majani mazuri hahitaji mume wala mke anajizalisha mwenyewe, anapata soko na ni dola elfu 25. Kwa hiyo ukienda Ghana ni soko kubwa sana kwenye maeneo hayo. Hivyo, naomba hili tatizo tusiogope kutafuta fursa ya mambo ambayo yapo wazi, tulizungumze wazi na vijana wapate ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumzia habari ya jimboni kwangu. Sisi kule jimboni tumejenga maboma tisa ya maabara za sekondari hayajamalizika kwa sababu nguvu za wananchi zimekuwa kubwa kwenye maeneo haya, tunaomba sasa maeneo yanayohusika waweze ku-support wananchi wa Jimbo la Bunda kwenye mambo ya maabara waweze kupata nafasi ya watoto wao kusoma sayansi ambapo kwa sasa sayansi inakuwa ngumu sana kuisoma kwa sababu maabara hazipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunalo tatizo la barabara, ambapo barabara ya kutoka Nyamswa kwenda Bunda haijatangazwa na ni muda mrefu sasa tumekuwa tukisema barabara hii itatangazwa itapata mkandarasi tunaomba Wizara inayohusika na wamesikia na Rais amekuja pale akasema itatangazwa hivi karibuni, lakini haijatangazwa. Vile vile barabara ya kutoka Sanzati-Mugumu - Nata haijatangazwa na Rais amefika pale akasema itatangazwa hivi karibuni. Kwa hiyo, tunaomba kwa wanaohusika urekebishaji wa mambo hayo uweze kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, daraja la Silolisimba Mgeta limekatika na Meneja wa TARURA Bunda amelifunga na sasa ni wiki moja. Tunaomba wanaohusika sasa waone namna ya kufungua ile barabara ili wananchi waweze kupeleka ng’ombe zao mnadani na watoto waende shule kwa sababu hali siyo nzuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa leo nilitaka kusema hayo tu. (Makofi)