Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Awali ya yote, nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia sote kukutana katika Bunge hili la bajeti na kutimiza wajibu wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, nitumie nafasi hii tena kumpongeza Mheshimiwa Rais na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kauli ambazo wamekuwa wakitoa zaidi ya mara moja, mara mbili juu ya namna ambavyo watendaji wa Serikali na Serikali nzima inatakiwa ku-act na ku-behave katika suala zima la uwekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaongelea mambo mawili. La kwanza nitaongelea suala la investment. Suala la pili nitakaloliongelea ni la kilimo. Ukitazama takwimu za World Bank, The Economic Update No.11 iliyotolewa mwaka huu, inaonesha kwamba idadi ya Watanzania walioongezeka katika umaskini toka mwaka 2012 mpaka leo ni Watanzania milioni mbili. Watanzania milioni mbili wameongezeka kwenda kwenye umaskini. Kwa nini? Nitaeleza baadaye.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia asilimia 60 ya population ya nchi yetu au mpaka 70 ipo katika sekta ya kilimo. Mipango yetu yote tunayofanya kama nchi na financing program zetu zote tunazozifanya kama nchi ni lazima ziangalie ni namna gani zina-improve productivity na kuhakikisha kunakuwa na masoko ya uhakika ya wakulima ili tuweze kuondoa watu wetu katika umaskini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukitazama financing ya sekta ya kilimo kwa miaka mitatu mfululizo, tunachowekeza katika sekta ya kilimo kinazidi kupungua kila mwaka. Tunachowekeza na kile tunachoki-disburse against bajeti yetu ya maendeleo, haviwiani. Sekta yetu ya kilimo inachangia asilimia 29 ya GDP ya taifa letu lakini inatengewa less than 5% ya development budget. Wakati huo huo population yetu inaongezeka kwa wastani wa asilimia 3, hili ni tatizo, ni lazima watu wataendelea kuongezeka kwenye umasikini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nini ushauri wangu katika hili? Hakuna njia tunayoweza kuondoa watu kutoka katika umaskini kama hatutofanya mambo matatu. La kwanza, ni lazima tuanzishe Price Stabilization Fund kwenye eneo la kilimo ili wakulima wanapokutana na mtikisiko wowote wa soko la dunia ama unpredictability kwenye bei za dunia tuna njia ya kuwaokoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kunapotokea hili tatizo, mimi ninazo takwimu za toka mwaka 2014 – 2017, zao la pamba msimu wa mwaka 2013 kwenda mwaka 2014 production ilishuka kwa asilimia 30; mwaka 2015 lilishuka kwa asilimia 17; mwaka 2016 lilishuka kwa asilimia 16; mwaka 2017 lilishuka kwa asilimia 18 na mwaka huu lime-grow kwa initiative iliyofanywa na Serikali. Zao la korosho ukiangalia toka mwaka 2014 lilikuwa lina negative trend lakini mwaka 2017/2018 zao hili lime-grow ni kwa sababu tuliwekeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu, moja, kama nchi ni lazima tuanzishe Price Stabilization Fund kwa ajili ya mazao ya kilimo. Mbili, ni lazima tuanzishe mfuko wa ku- subsidize inputs kwa sababu mazao tunayoyazalisha kwa ajili ya kwenda kwenye export sisi hatuna uwezo wa ku-control bei nje, tuna uwezo wa ku-control uzalishaji na quality. Sasa mzalishaji mfano wa mahindi, kama tutakapompa mbolea, viuatilifu hatutotoa ruzuku katika maeneo haya maana yake gharama ya uzalishaji itakuwa kubwa, soko halipo au halipo la uhakiki, matokeo yake mkulima huyu atakata tamaa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesoma mpango ambao umesomwa na Wizara ya Fedha ambao tutaujadili, ningeshauri katika misingi na maeneo makuu matano ambayo Wizara ya Fedha wamesema, eneo la kufungamanisha ukuaji wa uchumi na maendeleo ya watu, hapa wametaja suala la elimu, maji na afya ni lazima tuweke wazi (precisely) component ya kilimo, kwamba ni eneo muhimu la kufungamanisha uchumi na maendeleo ya watu ili liweze kupata priority. Kwa sababu tukianza kulijadili kwa staili hii tutaanza kulitengea fedha tunapokuwa na uwezo. Hili ni eneo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la pili ni la masoko, nini ushauri wangu? Tumeanzisha Tanzania Agricultural Development Bank. TADB kuna tatizo la structure kwa sababu TADB iko chini ya Wizara ya Fedha, Bodi ya Mazao mchanganyiko, NFRA na Bodi zingine ziko chini ya Wizara ya Kilimo, kuna suala la marketing ambalo liko chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara na kuna suala la investment ambalo liko chini ya Wizara ya Waziri Mkuu. Ushauri wangu ni lazima kutafutwe njia ya kutengeneza a strategic alliance kati ya hizi Wizara zote kwenye suala la marketing ya mazao ya wakulima ili Bodi ya Mazao Mchanganyiko kama tunaenda kwenye msimu waweze ku-plan nje kuna mahitaji ya mahindi kiasi gani, masoko yako wapi, Serikali isihitaji ku-finance, TADB awa-finance wanapokuwa wamepata contract za kuuza mazao nje. Hii itasaidia predictability ya mazao tunayozalisha. Tusipofanya namna hii, aje kiwanda cha magari na kadhalika, viwanda hivi havita-break even, havitaweza kuzalisha kwa sababu sehemu kubwa ya watu haina purchasing power. Hili ni jambo la pili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu ambalo nataka nishauri na mimi niipongeze Wizara ya Fedha nimeona kwenye mpango wameongelea uboreshaji wa mazingira wezeshi kwa uendeshaji wa biashara na uwekezaji. Lazima Serikalini watu wafahamu kwamba suala la mtu kuchukua shilingi mia moja yake kwenda kuiwekeza kwenye nchi au mji number one ni perception kwamba naamini shilingi mia yangu nayoenda kuiweka pale iko salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo Kariakoo is dead na mimi nimpongeze Waziri Mkuu alienda kukutana na wafanyabiashara wa Kariakoo. Nawaomba suala la Blue- print kama linahitaji mabadiliko ya sheria leteni tubadilishe. Suala la Blue-print kama linahitaji harmonization ndani ya Serikali ifanyike. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, World Bank wametoa ripoti, wamesema key areas ambazo zinatumbua sisi Tanzania kwenye suala la investment ni kwamba moja, kuna utitiri wa kodi ndogo ndogo. Mbili, hakuna simplicity kwenye suala la ulipaji wa kodi na tozo. Tatu, wanashauri kuwe kuna simplified system and predictable tax regime. Haya yatatusaidia watu kuja kuwekeza. Jamani, ambalo nataka nishauri na hapa Waheshimiwa Wabunge wengine wamesema, leo inaanzishwa Task Force inaenda Kariakoo pale inasimama, eti ile Task Force ina Polisi, haijui kukusanya kodi. Polisi kasomea wapi ukusanyaji wa kodi? Ina TAKUKURU; TAKUKURU kasomea wapi ukusanyaji wa kodi? Ina watu wanasemwa kutoka Idara nyeti za Serikali, ina watu wa TRA, na kadhalika. Kundi la watu limekaa pale Kariakoo, mtu kanunua mfuko wake anaambiwa leta TRA aah, hii ni feki huyu.

Mheshimiwa Naibu Spika, huyu mtu katoka Kongo anajuaje kama ile karatasi ya EFD mashine yake ni feki? Hawezi kujua, atabebwa, anawekwa Msimbazi Kituo cha Polisi. Next time haji, anaenda Uganda; anaenda nchi nyingine. Hii ni shida. Ni lazima suala la ukusanyaji kodi liachwe mkononi kwa watu waliosomea ukusanyaji wa kodi. Polisi wakafanye kazi yao, TAKUKURU wakafanye kazi yao. Hii ni dis-incentive.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo ukienda kwenye soko letu la hisa, trade volume imeshuka sana, share prices za share zilizoko kwenye soko la hisa zimeshuka. Kwa sababu gani? Sababu ni chache tu. Moja, there is no investors wanaoenda kununua na kuuza shares; wanaoenda kununua shares, watu wameshikilia share zao. Pili, maana yake hakuna surplus, hakuna fedha za ziada ambazo watu wanataka kuwekeza. Tatu, kuna kuwa na unpredictability. Kwa hiyo, tusipofanya haya mambo kuwa na sera ambazo ziko predictable katika suala la investment, hatuwezi kuondoka hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mwisho ambalo nataka nishauri, leo tumewekeza sana kwenye ndege, it is very good. Nami nataka niseme, uwekezaji wa ndege is not for itself, lakini uwekezaji wa ndege ni means to drive other sectors. Tumewekeza kwenye ndege, tumejenga viwanja vya ndege, nami nimshauri Mheshimiwa Waziri wa Fedha. Waziri wa Fedha ni lazima uwasainishe Wizara wa Tourism Performance Agreement, kwamba wanakuongezea tourists kiasi gani kurudisha investment uliyoifanya kwenye ndege? Ni lazima kwa sababu hizi ndege ambazo tumewekeza, tunajenga viwanja vya ndege kwa kasi sana, tunafungua nchi yetu, ni lazima tuweze kupata return kutokana na hii investment.

Mheshimiwa Naibu Spika, investment hii, hatutaki tuone ATCL; nami kwanza niseme tu wanasiasa, hebu nitajieni Africa Airline gani ina-make profit? Hakuna! They are making loss. It is not true. African Development Bank wame-predict Airline sector Africa globally ita-make 3 million US dollar loss, zote! Sasa hizi Airline zinafanya nini? Zinakuwa ni feeders za sector nyingine. Kwa hiyo, ni lazima sekta nyingine tuzitengenezee utaratibu wa kujua kwamba tumewekeza shilingi 100 kwenye ndege, wao wanaleta shilingi ngapi? Tusiseme tu tuna Bombardier tuna Dreamliner, tuna nini; ni lazima hizi ndege zitusaidie kukuza sekta nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, tunajenga reli. Mimi niseme hapa, nilisikitika sana. Tanzania imewekeza sana Kongo kwenye usalama. Tumewekeza sana. Askari wetu wamepoteza maisha yao. Sisi Rais wa Kongo kaapishwa, nilikuwa nafuatilia, wawakilishi wetu kama nchi wametua, wameenda kwenye kuapisha, wamegeuza.

Mheshimiwa Spika, Kenya katua Rais wa pale na delegation ya wafanyabiashara 60, wamekaa kusaini mikataba, kesho yake kaondoka. The first visit ya Rais wa Kongo is Kenya; and you know what? Wamesaini makubaliano ya Kenya itaenda ku-train civil servant wa Kongo. This is a forex. Katoka pale CEO round table ziliofanyaka Rwanda, kaenda Kigali three days. Naishauri Serikali, ni lazima tuwe business oriented. This is very important. Bila hivyo, Waziri wa Fedha hapa atakuja kudondoka na pressure. Tunaomba maji, tunaomba nini, he cannot do anything.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nashukuru. (Makofi)