Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI NDUGU PROF. MUSSA ASSAD, MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

Hon. Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI NDUGU PROF. MUSSA ASSAD, MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Naomba nianze kunukuu maneno ya Katiba ambayo Mwenyekiti wetu wa kudumu wa upande wa pili ameyatumia kwenye Ibara ya 18. Katiba hiyo ambayo ameitumia, ukisoma Ibara ya 30 nadhani uhuru una mipaka yake. Mfano mwingine mzuri, sioni cha ajabu. CAG sio mtu wa kwanza kulikosea heshima Bunge. Tumekuwa na Wakuu wa Mikoa, tumekuwa na Waheshimiwa Wabunge akina Mheshimiwa Ester Bulaya. Hata hivyo, walipoitwa kwenye Kamati walijieleza na wakomba radhi. Walipokuja humu ndani, baada ya kuwasikiliza tuliwasamehe na kazi zikaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, najuliza hii huruma inayotaka kuoneshwa humu Bungeni, hebu niwakumbushe, kuna watu akina Mheshimiwa Zitto walitumikia chama fulani kwa nguvu kubwa kukijenga, lakini walivyokiuka mipaka yao walifukuzwa juu kwa juu. Leo sisi kama Bunge tumetoa nafasi ya CAG kujitetea na kashindwa kuutumia uhuru wake, halafu tunaonesha huruma ya kazi gani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ingekuwa CAG ameitukana Serikali ambayo ndiyo iliyomteua ilikuwa siyo jukumu letu kuingilia hayo maamuzi, lakini Bunge, mimi nimeingia humu kwa kura 98,000. Mtu anakuja anasema ni dhaifu plus watu wangu, halafu tunamsamehe! Haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nami niwaombe Watanzania, kuna watu dhaifu humu ndani, tunawaelewa. Wawachambue waone kama wanahitaji kuwa dhaifu wawaoneshe huruma yao. Sisi ambao sio dhaifu kwa maelezo ya kamusi, tunaomba yaendelee maamuzi ya Kamati.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. (Makofi)