Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kusema kwamba tunaishi kwenye dunia ambayo ina rasilimali za kudumu na zinaisha. Ili nchi iweze kuendelea ni lazima sheria zote ambazo zinatungwa katika Taifa zielekeze kuzisimamia rasilimali hizo na kuziweka katika chain ambayo izitafanya ziwe endelevu. Katika kuwekeza kwenye rasilimali ambazo zina tabia ya kuisha, fedha ambazo zitapatika ni lazima ziwekezwe ili zikiisha basi pato la Taifa liweze kupatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitataja sehemu ambazo ni muhimu sana kuwekeza, kwanza, kuwekeza kwenye human capital kwa maana ya rasilimali watu na ndiyo ambacho Serikali inafanya inawekeza sana kwenye elimu. Pili, kuwekeza kwenye human made capital kwa maana ya miundombinu ndiyo maana unaona Serikali inawekeza kwenye Stiegler’s Gorge, treni, barabara, ndiyo kazi Serikali inafanya. Sehemu ya tatu ni kuwekeza kwenye innovation na technology, ugunduzi pamoja na teknolojia. Ugunduzi ninaozungumzia ni kuwekeza katika eneo litakalovumbua watu wenye uwezo wa kufikiri katika hali ya utupu, kukaa chini na kugundua. Leo Israel ni jagwa lakini kwa sababu watu wake wana uwezo wa kufikiri katika hali ya utupu, mimea inapewa dawa specifically siyo kurusha kama tunavyorusha sisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tuna hizi rasilimali zinazohisha na tunataka kuwekeza huko tujue wenzetu katika mataifa mengine rasilimali zao zimekwisha. Wamefika mahali sasa wanatoka nje ya mataifa yao kwenda kutafuta maeneo ya kuwekeza ili waweze kuhakikisha usalama wa nchi yao kiuchumi. Ndiyo maana utakuta baadhi wanaweza kutumia vyama vya siasa au mtu mmoja mmoja kuvuruga baadhi ya mambo ambayo yanawazuia wao kuwekeza kwenye rasilimali za Taifa husika. Ndiyo maana utaona…

T A A R I F A

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, Selasini unajua vizuri ni yule rafiki yako wa pale Moshi ame-supply vitu substandard. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana sisi tulipokuwa upande ule wa Selasini, Selasini akituongoza kwa sababu walishaweka mkakati…

KUHUSU UTARATIBU

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, Paroko nimepokea hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipokuwa upande ule walianza na mkakati wa kuhakikisha wanazuia Serikali yetu isiwekeze kwenye maeneo haya ya kimkakati. Tukajipanga namna ya kuzuia na kukwamisha Serikali ili isiwekeze katika eneo hilo. Mwenzetu Mheshimiwa Tundu Lissu akaonyesha kuwa kinara wa kuzuia hilo, yakatokea mambo mawili. Jambo la kwanza ikaonekana kwamba anatengeneza umaarufu binafsi lakini ya pili kwa sababu ni watu ambao wamepanga kuuza hili Taifa wakatuma watu wakampiga Tundu Lissu na kumuumiza… (Makofi)

WABUNGE FULANI: Ooh, ooh.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo tayari kuthibitisha. Namna ambayo nitathibitisha kwanza leo tu jioni hii nitatoka nje, isisemekane nimesema twende Mahakamani lakini CHADEMA waniletee matumizi yao yote ya ruzuku na hela wanazotoa nje wanatumia kufadhili nini? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilikuwa Daktari niliyewakilisha CHADEMA kwenye postmortem ya mabomu ya Arusha nilipotoka nikaiambia CHADEMA, Mheshimiwa Mbowe, Mheshimiwa Lema na Mheshimiwa Selasini walikuwepo ni Mkutano wa Kanda, kwa sababu kilio chetu tunasema hatuamini Serikali kwenye kuchunguza kuna vitu nimeviiba huko ndani twendeni tupeleke kwa Mkemia Mkuu wa Afrika Kusini walikataa, waseme kwa nini walikataa na walikuwa na ruzuku. Wanapinga suala la Mheshimiwa Tundu Lissu, Chacha Wangwe kilimtokea nini baada ya kutaka Uenyekiti? (Makofi)

T A A R I F A

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, anasahau kilio alichotoka kulia hapa Serikali isaidie, mimi nilikuwa kada mwaminifu, nikafanya kazi za chama lakini walinikwamisha wao, nikagundua kwamba wanajua kinachoendelea. Mnajua Mheshimiwa Zitto leo asingekuwa hai kwa kilichomtokea kama siyo Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi kumlinda. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru aliyenijibu hapa ni mmojawapo wa wale waliokuwa wanatengeneza njama za kumng’oa Mbowe. Kwa hiyo, kuna uthibitisho dhahiri hapa kwamba huko kuna mafia wa kutosha. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaeleze tu…

T A A R I F A

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, napokea taarifa kwa sababu tulikuwa pamoja na tulikimbia umafia kwa ajili ya nchi yetu. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kulikuwa na plan namba moja ya kuzuia Serikali isifanye kazi, katikati ya plan namba moja Lissu akapigwa risasi ili kusisimua watu waivuruge Serikali yetu. Plan namba mbili ndiyo inaendelea Ulaya ambayo ni mwendelezo wa kufadhiliwa na wale watu wachafu. Mimi sisemi kuwa kuna nchi yoyote inafadhali ila ni watu wachafu ambao ni wezi wa rasilimali za kidunia. Tunataka kuwapa taarifa kuwa hakuna rasilimali ya Tanzania mtakayoweza kuipekea nje ilhali Watanzania wapo na leo tunawaambia ukweli. Tanzania haiuzwi kwa makubaliano ya ninyi kufika Ikulu, mkifika Ikulu mtasimamia nini? (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)