Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Saed Ahmed Kubenea

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Ubungo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika hoja ambazo ziko mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze mchango wangu kwa kunukuu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sehemu ya Utangulizi ambayo inasema: “Kwa kuwa sisi Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, undugu na amani. Na kwa kuwa misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia ambayo Serikali yake husimamiwa na Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi, na pia wenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimenukuu msingi huu wa Katiba nikirejea kesi mbalimbali ambazo zimepelekwa Mahakamani na zimecheleweshwa kwa makusudi kabisa. Moja ya kesi ambayo nataka niitolee mfano ni ya Mheshimiwa Joseph Mbilinyi, Mbunge wa Mbeya Mjini ambaye alifungwa na Mahakama ya Mkoa wa Mbeya, akakata rufaa kwenda Mahakama Kuu na aliomba awe nje kwa dhamana wakati shauri lake linasikilizwa lakini Mheshimiwa Mbilinyi alikaa gerezani kwa kipindi chote cha kifungo chake hadi pale alipotoka baada ya kupata msamaha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katiba yetu inasema Mahakama itende haki bila kuangalia sura ya mtu lakini wapo watu ambao wamekosa haki zao kwa makusudi kabisa kwa utaratibu ambao Mahakama imeshindwa kuwapa haki hizo. Taarifa zilizopo ni kwamba Jaji aliyekuwa Incharge kwenye kesi ya Mheshimiwa Mbilinyi alikiri kwamba alishinikizwa kuendelea na shauri lake kulipeleka mbele.

MWENYEKITI: Mheshimiwa kubenea haya maneno unaweza ukayathibitisha?

KUHUSU UTARATIBU

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Bunge hili lilipokea Muswada wa Mobile Court, uliletwa kwenye Kamati ya Katiba na Sheria, Serikali katika mvutano wa adhabu ambazo zilikuwa zimependekezwa katika Mahakama hiyo ikaondoa ule Muswada. Hata hivyo, juzi wakati wa uzinduzi wa Siku ya Sheria tumesikia kwamba Mahakama imezindua Mobile Court.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya mashaka ya Wabunge yalikuwa Mobile Court ina gharama kubwa sana. Gari moja lilikadiriwa kuwa na thamani kati ya shilingi milioni 200 mpaka milioni 490. Tukasema gharama za kuendesha Mobile Court ambazo ni mkopo kutoka Benki ya Dunia ni kubwa kuliko tukiamua kujenga Mahakama za Kata. Pia tukasema katika baadhi ya maeneo gari hili haliwezi kufika na tukatoa mfano kwa Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe, kule juu milimani, gari hili la Mobile Court haliwezi likafika. Lingine lilikuwa ni eneo la maamuzi yenyewe na hasa katika eneo la fine ambazo zitaenda kutozwa kule na haki ya watu kupewa wakili na kusikilizwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Muswada unaletwa Bungeni tayari tenda au magari yalishaagizwa kutoka nje. Kwa hiyo, Bunge lilikuwa linatumika kuhalalisha kitu ambacho tayari kilikuwa kimeshafanyika.

T A A R I F A

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namheshimu sana kaka yangu, rafiki yangu, Mheshimiwa Mwakasaka, nikizungumzia Kamati ya Bunge nazungumzia Bunge Dogo. Nimesema Muswada ulikuja kwenye Kamati ya Katiba na Sheria na ukaondolewa na Serikali, sasa sijui, aah, naomba niendelee tu.

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ulinde muda wangu.

T A A R I F A

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson, alikuwa anazungumza hapa juzi akasema sisi Wabunge tuwe wavumilivu, tuwe tunasikiliza na wenzetu, usikilize kile ambacho pengine wewe hutaki kukisikia. Huyu mwenyewe hapo nje alikuwa analalamika na wenzake wawili na wenzake watasimama sasa hivi kwamba Rais Magufuli hasikilizi watu, sasa wewe unapata wapi moral authority ya kuniambia mimi. Kwa hiyo, taarifa yake nimeikataa.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Ibara ya 74(7) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inazungumzia juu ya uwepo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo tunayo sasa imeundwa na kifungu cha 6(1) cha Sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Na.1 ya mwaka 85 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2010.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia muundo na mfumo wa Tume yetu ya Taifa ya Uchaguzi katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu ujao na jinsi Wakurugenzi wa Halmashauri ambao wanakatazwa na Katiba hii kwamba watu wanaojihusisha na vyama vya siasa (makada) wasiwe wasimamizi wa uchaguzi lakini ukiangalia huko chini muundo wa Tume, ukiacha pale juu unatutia mashaka kwamba tunaweza tukaenda kwenye uchaguzi mkuu wa 2020 tukiwa na amani na usalama. Niishauri Serikali na niiombe sana kwamba ifanye marekebisho ya Tume yetu ya Uchaguzi ili yale mambo ambayo yametokea Zanzibar mwaka 2001, yametokea Kenya na katika mataifa mengine yasije yakatupata na sisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina picha za Wakurugenzi wa Halmashauri ambao walikuwa makada wa CCM na walikuwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa. Wengine asubuhi wanakuwa makada wa CCM na mchana wanaenda kusimamia uchaguzi, kinyume na Katiba yetu, kinyume na Sheria ya Uchaguzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hatua ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Mheshimiwa Jecha Salim Jecha, kuamua tu binafsi kufuta uchaguzi wa tarehe 25 Oktoba…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)