Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

NAIBU WAZIRI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba niungane na Waheshimiwa Wabunge waliopata fursa ya kuchangia, kwanza kwa kuzipongeza Kamati zote tatu kwa taarifa ambazo wamezitoa, ni taarifa nzuri sana.

Mheshimiwa Spika, kipekee naomba nipongeze Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa, ikiongozwa na Dkt. Jasson Rweikiza na Makamu wake na wajumbe wote kwa ujumla. Naomba nitoe takwimu chache, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, jumla tulipata bajeti tuliyopitishiwa na Bunge lako Tukufu Sh.1,803,400,959,500 na katika hizo, naomba niendelee kumshukuru Mheshimiwa Rais, tumeweza kupata pesa kwa ajili ya shughuli za maendeleo jumla ya Sh.856,560,441,937. Hii ni sawasawa na asilimia 47.5, hiyo si haba na fedha zote hizo zimeenda kwa ajili ya shughuli za maendelo.

Mheshimiwa Spika, mgawanyo wa fedha hizo, jumla ya Sh.141,605,849,192 zimepokelewa ofisi kuu kwa maana ya Wizarani na kati ya fedha ambazo ilikuwa jumla ya Sh.345,113,541,000, lakini bilioni 40 zimepokelewa kwenda kwenye Serikali za Tawala za Mikoa; kati ya bajeti ya Sh.93,184,414,000, jumla ya Sh.694,643,380,250 zimepokelewa kwenye Halmashauri za Serikali za Mitaa, kati ya jumla ya Sh. 1,365,107,004,500 zilizoidhinishwa na Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Spika, tunakushukuru sana, tunashukuru Wizara ya Fedha, hizi fedha zote zimeenda kufanya kazi za maendeleo. Kati ya fedha hizo, iko jumla ya bilioni mia moja nukta tano ambazo ni za kujenga hospitali 67 katika Halmashauri zetu. Tumepanga katika bajeti inayokuja tunaenda kuongeza hospitali 27 katika zile 67, kwa hiyo ukijumlisha utaona namna kazi nzuri ambayo inafanywa na Serikali ya CCM chini ya Uongozi wa Rais wetu, mpendwa Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama hiyo haitoshi zimeenda shilingi bilioni 23 kwa ajili ya kujenga Ofisi zetu za Halmashauri; lakini pia zimeenda shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kununua boti; zimeenda shilingi bilioni 11 kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya Jimbo, Waheshimiwa Wabunge ni wanufaika na naamini fedha hizo zitakuwa zimetumika kwenda kuchochea kwenye shughuli za maendeleo.

Mheshimiwa Spika, kuna hoja ambazo zimeibuka ambazo ni vizuri tukatolea ufafanuzi. Hoja ya kwanza inahusu suala zima la TARURA, tunaomba tupokee pongezi ambazo Waheshimiwa Wabunge wote waliopata fursa ya kuchangia wamepongeza kazi nzuri ambayo inafanywa na TARURA, lakini kuna upungufu ambao wanataka uboreshwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mgawanyo wa fedha, asilimia 70 kwa 30 kwa mujibu wa Sheria iliyopo na TARURA tangu imeanzishwa ndio ina miaka miwili, kuna mapitio ambayo yanafanyika ili tupate formula itakayokuwa nzuri, baada ya kujua mtandao mzima wa barabara na kiasi cha fedha ambacho kinatolewa, tujue namna gani ambayo tutawezesha chombo hiki kizuri ambacho kina upungufu mchache lakini Waheshimiwa Wabunge wengi wamesifia juu ya utendaji kazi wa TARURA. Kwa hiyo, tunaomba tuendelee kukiunga mkono.

Mheshimiwa Spika, hapa Waheshimiwa Wabunge wameongelea kuhusiana na suala la kuripoti; ni kweli, azma ya kuanzishwa kwa TARURA wengi tunajua, wakati ule, ilikuwa kila Mbunge ambaye sasa akirudi kule, Diwani anataka angalau wapate hata kilometa mbili, kwa hiyo, value for money kwa ujumla wake, ilikuwa haionekani, tunaamini kabisa, iko haja ya Waheshimiwa kushiriki katika kutoa mapendekezo, TARURA waende kutekeleza.

Mheshimiwa Spika, yako mengi na dakika tano ni chache, hivyo, naunga mkono hoja. (Makofi)