Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza nichukue nafasi hii kuunga mkono hoja za Kamati zote tatu. Pili, niwapongeze Mawaziri wa Wizara zote tatu kwa kazi nzuri wanazofanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kumpongeza tena Waziri wa Michezo, takribani miezi minne nilitoa hoja kuhusu Uwanja wa Taifa kutokuwa na sehemu ya kivuli kama mvua zitanyesha. Immediately kazi inafaywa na nafikiri mechi ya tarehe 16 watu tunaokaa katika maeneo yale hata ikija mvua tutakuwa tunasheherekea ushindi wa timu yoyote itakayojaliwa na Mwenyezi Mungu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, FIFA ina standard ya viwanja ndiyo maana inaleta fedha kutengeneza viwanja katika miradi ya FIFA. Vipo viwanja vinachezewa Premium League vina hali mbaya sana, vinaharibu ubora na viwango. Mfano jana, kwa dhati kabisa nasema, Uwanja wa Singida ambapo jana Club za Yanga na Singida United wamecheza hauna sifa wa kuchezewa mashindano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimwa Waziri, najua TFF ni watu independent lakini ninyi ndiyo custodian na ndiyo mnasimamia viwango vya Watanzania. Timu ambazo zipo kwenye Premium League na viwanja vyao ni vibaya wahamishiwe viwanja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni jambo la kusikitisha sana jana kuona klabu kubwa kama Dar Young Africans inashindwa kucheza kandanda yake. Naomba wanaohusika walione hili kwa sababu kwenye mpira kuna formation, kuna diagonal attack, diagonal defence, kama kiwanja kibaya, maana kama kule Mbondole kuna kiwanja ambapo kipa wa huku hamuoni kipa wa kule, wanaulizana vipi huko? (Kicheko/Makofi)

MBUNGE FULANI: Ngapi huko?

T A A R I F A

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, nafikiri Mheshimiwa Waziri amenielewa.

MBUNGE FULANI: Taarifa umeipokea?

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Kwa Morogoro nimeipokea. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, mchango wangu unajikita kwenye masuala ya viwanja ambavyo havina ubora, Serikali iingilie kati iambie TFF viwango vya wachezaji vinakufa…

T A A R I F A

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, hata usinihoji, sipokei taarifa yake. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, viwanja hivi ndiyo vinatoa ubora wa wachezaji wa Timu ya Taifa, viwanja vibovu vyote pamoja na cha Singida na viwanja vingine vya timu zinazoshiriki Premium League kama Mkwakwani Tanga, vilabu vile vihamishiwe kwenye viwanja vingine ili ubora na viwango vya mpira viweze kupatikana Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)