Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kwa unyeyekevu kabisa nianze kwa kumpongeza…

SPIKA: Dakika 10 eeh.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, sawa na ahsante sana. Naomba nianze kwa kumpongeza sana Chief Whip wa Opposition, Mheshimiwa Tundu Antiphas Mughway Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki na Rais Mstaafu wa Tanganyika Law Society – TLS. Nampongeza kwa ziara zake za kimataifa kuelezea hali halisi ya kinachoendelea nchini kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Lissu alimiminiwa risasi 38 na 16 ziliingia mwilini. Katika hali ya kawaida ilibidi alegee na kurudi nyuma, lakini pamoja na kwamba, bado yuko kwenye matibabu amechukua jukumu la kuzunguka na kupaza sauti ili dunia ijue kwamba… (Makofi)

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi walikuwa wanauliza ukurasa wa ngapi wa taarifa?

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, kama wao wanavyoanza na pongezi tu kwa mtukufu. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Spika, muda wangu. Kwa hiyo, kwa mtu ambaye risasi 16 zimeingia ambaye alitakiwa alegee, lakini amenyanyuka na anazunguka kuilezea dunia kwamba, Tanzania, Tanzania ambayo ilikuwa ni kitovu cha amani Kusini mwa Jangwa la Sahara, hivi sasa imekuwa ni authoritarian regime. Tuelewane kitu kimoja, Serikali siyo Taifa kuikosoa Serikali siyo kulichafua Taifa na kuikosoa Serikali siyo kuitukana Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa niende kwenye hoja, kwanza naunga mkono ripoti ya Kamati yetu ya Huduma na Maendeleo ya Jamii. Nianze na habari na utawala bora. Kwanza Mungu atuondolee kabisa balaa la pepo la kuongeza muda wa utawala, ni tabia na mawazo ya kidikteta moja kwa moja, iwe kwenye Ubunge au kwenye Urais. Maana naona hii trend mlianza kama utani lakini sasa hivi mnakuwa serious, naamini mnahitaji maombi na tutapiga magoti tuwaombee ili msiliingize Taifa huko mnakotaka kulipeleka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwapongeze CCM Habari kwa kumilikishwa Chanel Ten na Magic FM. Naamini kwa hatua hii sasa mtaiacha TBC ibaki kuwa TV ya umma.

T A A R I F A

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, siipokei taarifa yake, actually alichoniambia Keissy ni kwamba anataka ni m-support hoja yake ya kutaka bangi iruhusiwe na nimemkatalia na hii anayo toka Bunge lililopita. Kwa hiyo, hiyo taarifa yake siichukui. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, naipongeza CCM kwa kukabidhiwa Channel Ten na Magic FM. Sijui mmepewa, mmenunua na kwa utaratibu gani kwa sababu najua makampuni yanapouzwa upo utaratibu lakini tumeona tu ghafla watu wanakabidhiwa vyombo vya habari. Tunaamini sasa mtaiacha TBC ibaki kuwa TV ya umma ili mbaki na vyombo vyenu ambavyo mnavyo hivi sasa, muiache TBC kuwa televisheni ya umma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimemuona Mwenyekiti wa Taifa katoa shilingi milioni 200 kuboresha Channel Ten na Magic FM, wananchi wa Mbeya Mjini wananipigia wanasema Mheshimiwa hizo fedha shilingi milioni 200 zilizotoka ni fedha za CCM, fedha za Serikali Hazina au zinatoka wapi? Tunavyofahamu Mwenyekiti wa CCM Taifa kazi yake ya Urais mshahara wake ni shilingi milioni 9 tu. Sasa wananchi wanajiuliza anatoa wapi mamilioni anayoyagawa kila sehemu anakopita wakati mchahara wake Rais mnyonge ni shilingi milioni 9 tu. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, walisema ni Rais katoa, kwa hiyo, kama ni Mwenyekiti ndiyo mnanipa taarifa basi naelewa sasa kumbe ni hela za Chama cha Mapinduzi na siyo hela za mtu binafsi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye afya, ripoti inaonyesha kwamba rufaa za nje zimepungua kutoka 114 takribani kwa mwaka mpaka 38. Kwangu mimi na nilivyofuatilia kwenye Kamati hii siyo success story kwa sababu watu wanakufa sana. Hivi sasa Madaktari wanaogopa kutoa rufaa kwa sababu ya kuangalia mtazamo wa kisiasa unataka nini kwamba hatutaki kupeleka watu nje. Lazima tukubali kwamba hatuna mabigwa wala hatuna vifaa vya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sometime, narudia tena sametime Muhimbili pale nimekaa zaidi ya mwezi mmoja na nusu hata mtungi wa gesi oxygen inabidi ibadilishwe yaani kuna mgonjwa hapa amelala, amewekewa mtungi, mgonjwa mwingine kule anataka kuwekewa mtungi inabidi watu wamkatie nurse ili mtungi uhamishwe wanasema huyu amepumua kidogo tutamletea tena baadaye. Kwa hiyo, katika hali kama hiyo huwezi….

T A A R I F A

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri anafahamu vizuri ana struggle na hapa tunachofanya ni kumsaidia kwa sababu yeye hawezi kutamka haya tunayotamka atatumbuliwa. It is not about you Madam Minister it is about the Nation, hatukusaidii wewe tunalisaidia Taifa hapa, hakuna vifaa na wataalam wa kutosha, watu wakufa.

T A A R I F A

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, nilindie muda wangu vinginevyo sasa mimi katika hili Bunge nitakuwa sichangii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haya mambo tunaongea tuko serious, kama Mzee Kingunge angepelekwa nje kutibiwa pengine leo hii tungekuwa na Mzee Kingunge. Huwezi kumweka Mzee Kingunge mwezi mzima hospitali ya rufaa, ukishamweka wiki moja hajapata nafuu ujue kuna tatizo mpeleke kwenye weledi wa juu zaidi. Mpaka leo mnashindwaje kumpeleka Mheshimiwa Salim Mohamed Salim, Waziri Mkuu Mstaafu, Makamu wa Pili wa Rais, unashindwaje kumpeleka kutibiwa nje pamoja na wananchi wengine wenye mahitaji? (Makofi)

T A A R I F A

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, niwaombe sana hawa wanaosimama kutoa taarifa, hii nchi siyo ya baba yao wala hili Bunge siyo la mama yao, hili Bunge ni la Taifa na hapa tunajadili suala la Taifa.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Spika,
kuhusu utaratibu.

SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi, nakuomba sana u-withdraw hayo uliyoyasema.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): Kabisa.

SPIKA: Kwa Wabunge wenzako, ndugu zako na Waheshimiwa wenzako.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, kwa sababu tunaheshimiana I am withdrawing this lakini ujumbe umeshafika, habari ndiyo hiyo.

SPIKA: Ahsante sana. Tunaendelea na Mheshimiwa Ritta Kabati.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Muda wangu haujaisha hata kengele ya pili katika mustakabali wako haujaisha Mheshimiwa.