Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Augustine Vuma Holle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kukushukuru sana kwa kunipa nafasi hii adimu ya mimi kuweza kuchangia kwenye hotuba ya Waziri wa Katiba na Sheria, lakini pia na hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nipende kueleza masikitiko yangu kwa hali ambayo imejitokeza jioni ya leo. Ama kweli hii imedhihirisha kwamba mkuki kwa nguruwe lakini kwa binadamu ni mchungu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niende kwenye hoja, kwanza napenda kumshukuru Mzee wangu Mheshimiwa Dkt. Harrison Mwakyembe kwa kutuonyesha umahiri wake leo tena kwa kupitia hotuba yake ambayo ameitoa hapa. Napenda kulikumbusha Bunge hili kwamba umahiri wa Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe haujaanza leo, huyu ndiye aliyeongoza Kamati ambayo ilimuondoa madarakani fisadi papa namba moja Ndugu Edward Ngoyai Lowassa. Mzee Mwakyembe tunakushukuru sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe yako mambo machache ya kukushauri tu mzee wangu. Suala la kwanza ni Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2006…
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Kifungu 32(1), nanukuu, kinasema; ―Mfanyakazi atakuwa na haki ya likizo ya ugonjwa angalau siku 126 kwa kila mzunguko wa likizo.‖
Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili limeleta utata wakati mwingine kwa sababu wako wagonjwa ambao wameugua zaidi ya muda huu. Naomba sana kipengele hiki kiweze kurekebishwa ili watu wapate nafasi ya kuweza kutibiwa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni la wafanyakazi wa migodini. Watu hawa wamekuwa wakifanya kazi ngumu na wakati mwingine kulingana na mazingira duni ya migodini wamekuwa wakipata shida au matatizo ya kiafya na mara baada ya kupata matatizo ya kiafya huwa wanaachwa na waajiri wao na hatimaye wanakuwa maskini wakubwa sana. Kwa hiyo, ningeomba sana Mheshimiwa Waziri atakapokuja kwenye majumuisho hili nalo alizungumzie. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimejikita tena kwenye hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni…
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia ukurasa wa 11, Mheshimiwa Tundu Lissu anasema kunyamazisha upinzani na kukaribisha udikteta. Labda niwakumbushe watu hawa kwamba upinzani umejiua wenyewe yaani wamejikaanga kwa mafuta yao wenyewe. Moja, wamejikaanga kwa unafiki wao uliopitiliza, nitasema hapa ambao hasa umeongozwa na huyu huyu ambaye ni Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria.
KUHUSU UTARATIBU...
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niseme tu kwamba kwa taarifa zilizozagaa na ambazo kila Mtanzania anazifahamu...
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kwamba wagonjwa wa namna hii kwao wako wengi, mbona Mheshimiwa Mnyika yuko Muhimbili naye anatibiwa hivyo hivyo tu.
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba kwa mujibu wa Kanuni nifute kauli hiyo ya Mirembe na naomba kuendelea na unilindie muda wangu. (Makofi)
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nilisema hayo kwamba nimejiridhisha na kauli hizo za mtaani kwa sababu moja ya unafiki…
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mtu huyu amekuwa ni mnafiki namba moja katika nchi hii. Nitathibitisha unafiki na uongo wake.
Kwanza wakati anachangia hapa amesema eti anashangaa kwa nini Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania hajastaafu wakati aliosoma nao wamestaafu, anashindwa kujua kwamba siyo kila unayesoma naye umri wake ni sawa.
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Amesema aliosoma nao. Wakati mimi nasoma nimesoma na watu ambao wana umri wa baba yangu lakini mtu huyu ni msomi na anajua mambo yote haya anaamua kupotosha Taifa kupitia chombo kitakatifu cha Bunge kwa makusudi kabisa. Ndiyo maana nasema unafiki huu unanirejesha kwenye hizi rumors ambazo nimesikia mtaani.
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hilo nimeshafuta na mimi naendelea na mchango wangu. Sasa kama unaniambia kwamba niache kuchangia kwa kumzungumzia mtu huyu…
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Hapa nafanya hivyo ili kuweka record clear, kwa namna ambavyo amepotosha Bunge, kwa namna ambavyo …
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba unilindie muda wangu. Wewe unataka nini?
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nilindwe kwa mujibu wa Kanuni. Nimekuja hapa kwa mujibu wa Kanuni.